EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Thursday, August 14, 2014

Manispaa ya Iringa kutekeleza miradi ya maendeleo zaidi ya 4.7bn/-


Katibu wa Baraza la Madiwani Manispaa ya Iringa, Theresia Mahongo
ambaye pia ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa akisoma taarifa
muhtasari wa  utekelezaji wa shughuli za maendeleo  kwa kipindi chajulai hadi juni 2013/14.
 
NA MATHIAS CANAL.

IRINGAHalmashauri ya Manispaa ya Iringa katika mwaka wa fedha 2013/14
ilipanga kutekeleza miradi ya maendeleo yenye thamani ya
Tsh.4,723,360,853/=, kati ya fedha hizo Tsh.3,451,638,853 zilikuwa ni
ruzuku kutoka serikali kuu na wafadhili, na Tsh.1,271,722,000
zilitarajiwa kuchangiwa na Halmashauri kutokana na vyanzo vyake vya
ndani vya mapato.

: Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani Manispaa ya Iringa Amani
Mwamwindi (mwenye joho jekundu) ambaye pia ni Meya wa Manispaa
ya Iringa akihutubia wajumbe wakati wa kikao cha baraza hilo jana.

Michango ya wananchi na nguvu kazi katika kusaidia utekelezaji wa
miradi hiyo katika maeneo yao ilitarajiwa kufikia jumla ya Tsh.
266,398,000. Bajeti hiyo ilizingatia maelekezo, sera na miongozo kama
ilivyokuwa imetolewa na serikali.
Mhe. Mwenyekiti, Hadi kufikia Juni 2013/2014, Halmashauri ilikuwa
imepokea fedha za Ruzuku ya Miradi ya Maendeleo jumla ya
Tsh.3,646,883,588 sawa na asilimia 77 ya makadirio, kati ya fedha hizo
Tsh.3,443,844,897 sawa na asilimia 95 ya fedha zilizopokelewa
zimetumika katika shughuli mbalimbali za miradi ya maendeleo.

Wajumbe wa Baraza la Madiwani Manispaa ya Iringa wakifuatilia
kikao kwa umakini.

Miradi iliyopokea fedha ni pamoja na mfuko wa Barabara
Tsh.1,955,611,978, Mradi wa maji safi na usafi wa mazingira (NRWSSP)
Tsh.677,230,287, programu ya kuendeleza elimu ya sekondari (SEDP)
Tsh.92,215,124, Elimu msingi (PEDP) Tsh. 43,144,993, Kilimo (ASDP)
Tsh. 7,800,000, Mfuko wa jimbo Tsh.30,656,570, Mfuko wa pamoja wa
Afya Tsh.247,560,000, TACAIDS Tsh. 71,153,580, Ruzuku ya miradi ya
maendeleo (CDG)Tsh.108,090,000  na Tsh.410,505,056 zilipokelewa kwa
ajili ya fedha za kuendeleza mji (ULGSP).
Hata hivyo miradi mbalimbali iliendelea kutekelezwa kwa fedha
zilizovuka mwaka jumla ya Tsh.1,635,149,155, ambapo hadi kufikia Juni
2014 salio hili lilikuwa Tsh.1,122,017,019 kwa ajili ya mradi maji safi na
usafi wa mazingira Tsh.276,796,726, mfuko wa barabara
Tsh.783,456,167 na fedha za Mradi wa kuendeleza Mji (ULGSP) Ths.
61,764,126.

No comments:

Post a Comment