EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Thursday, August 14, 2014

JUMUIYA YA MADOLA YAITAKA RIPOTI YA TANZANIA KWA MICHUANO HIYO KUBADILISHWA LA SIVYO ITATOBOA SIRI YA NCHI HIYO KATIKA MICHUANO ILIYOMALIZIKA

NA NYEMO MALECELA
VYAMA vya michezo iliyoshiriki michuano ya Jumuiya Madola vimesema endapo ripoti ya meneja wa timu ya Tanzania, Mwarami Mchume haitabainisha ukweli wa yale yaliyojitokeza katika michuano hiyo, vitatoboa siri kwa Watanzania.
 Wakizungumza na SWACOTZ FORUM jana kwa nyakati tofauti viongozi wa vyama vya michezo hiyo, walisema wanasubiri ripoti ya Mwarami ili waweze kupasua jipu na endapo haitasema ukweli basi wao wataungana na kuitisha mkutano utakaoleza ukweli wa yale yaliyotokea.


Rais wa Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT), Ruta Rwakatale alisema wao tayari wameongea na mabondia walioshiriki michuano hiyo ambapo wameoanisha maelezo yao na ripoti ya kocha Jonasi Mwakipesile aliyeambatana nao na kujua sababu zilizopelekea kushindwa kupata medali.

“Tunasubiri ripoti ya meneja wa timu, ikitofautiana na yale tuliyoelezwa na kocha na mabondia tutaeleza ukweli maana tunayo mambo mengi yaliyosababisha tukose medali kwani pointi walizozipata mabondia wetu zinaonyesha ni kiasi gani tuliwaandaa vizuri,” alisema.

Nao makocha wa judo, Zaidi Hamisi, Ramadhan Namkoveka (kuogelea) na Ramadhan Othman (mpira wa meza) wamesema wanasubiri ripoti hiyo ili waeleze ukweli.

“Tunasisitiza ripoti ya meneja inatakiwa ieleze ukweli maana kuna mambo mengi yaliyosababisha sisi kushindwa kufanya vizuri na endapo itaficha chochote sisi tutaeleza ukweli ili Serikali itambue kuwa viongozi wa wizara ya michezo wameshindwa kuwajibika,” alisema.

No comments:

Post a Comment