MICHUANO ya soka kwa
timu maalum za mazoezi ya viungo zinazojulikana kama ‘Jogging’ inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Mei 10 mwaka
huu katika Uwanja wa Karume, jijini
Dar es Salaam.
wanaume kazini hapo wakikatisha katika kati ya mji na mazezi yao
Mashindano hayo yanayoandaliwa na Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) kwa kushirikiana na wabunge wa Ilala, Kinondoni na Temeke yatahusisha jumla ya timu 95 kutoka mkoani humu.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Mashindano hayo, Marijani Rajab, alisema lengo la mashindano hayo ni kuwakutanisha wanamichezo wa jijini Dar es Salaam ili kutafuta namna ya kuendeleza mchezo huo.
baadhi ya timu zikifanya mazoezi ya kukimbia
Alisema mshindi wa kwanza atajinyakulia pikipiki ya miguu mitatu, wakati yule pili ataondoka na bodaboda bila kusahau mshindi wa tatu atakayepewa zawadi itakayojulikana baadaye.
“Kutokana na ugeni wa mashindano haya tumeona bora tuanze na
timu za wanaume, ila tunaamini mwakani wanawake pia watashiriki kwa namna moja
ama nyingine,
mara baada ya kumaliza tutaanza mikakati ya kuhamasisha wanawake ili nao waweze kushiriki na kuongeza
hamasa ndani na nje ya mkoa,”alisema
wakati huo huo, ametowa wito kwa vilabu vingine kujitokeza na kuthibisha kushriki kwani hadi hivi sasa ni Camp za Jogging 45 ndizo zilizothibisha kushiriki,na mwisho wa kuthibisha ni Hiyo mei 10 siku ya ufunguzi.
wakati huo huo, ametowa wito kwa vilabu vingine kujitokeza na kuthibisha kushriki kwani hadi hivi sasa ni Camp za Jogging 45 ndizo zilizothibisha kushiriki,na mwisho wa kuthibisha ni Hiyo mei 10 siku ya ufunguzi.
No comments:
Post a Comment