EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Saturday, May 3, 2014

Wanaotemwa Azam FC hawa hapa


NYOTA sita wa mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Azam FC wamekalia kuti kavu baada ya kupigiwa mstari mwekundu wa kutohitajika katika kikosi cha timu hiyo msimu ujao.



Chanzo cha habari kutoka ndani ya uongozi wa Azam FC, kimewataja nyota waliopigiwa mstari huo kuwa ni Ibrahim Mwaipopo, ambaye amekuwa majeruhi kwa muda mrefu, Jabir Aziz na Seif Karihe ambao watapelekwa kwa mkopo moja ya klabu za Ligi Kuu.

Kilieleza uongozi wa Azam FC bado unatafakari Karihe aende timu gani ambayo itamsaidia kuimarisha kiwango chake, kwa kuwa ni miongoni mwa wachezaji ambao timu hiyo ina malengo naye ya muda mrefu.

Nyota wengine wanaotemwa ni Malika Ndeule, Kipre Bolou, Ismail Kone na Lackson Kakolaki ambaye atapelekwa shule kusomea ukocha kwa ajili ya kuandaliwa kuifundisha timu ya vijana ya klabu hiyo.
Tayari Azam ipo katika mchakato wa kuvunja mkataba na Bolou na Kone ambao ni raia wa Ivory Coast yakiwa ni mapendekezo ya kocha wao, Joseph Omog baada ya kuangalia upungufu wa kikosi chake na uhitaji wa nyota wapya kujiwinda na michuano ya kimataifa na Ligi Kuu.
“Sasa tunatakiwa kujipanga kimataifa kwa kufanyia kazi dosari zilizojitokeza kwa kuwapunguza na kuongeza wachezaji watakaosaidia timu kwa ajili ya safari ya kutetea ubingwa wetu na ushiriki wa michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika,” alisema.
Baadhi ya wachezaji waliomaliza mikataba yao lakini bado wana nafasi katika kikosi cha timu hiyo baada ya kumkuna Omog kwa kiwango chao ni mshambuliaji, Gaudence Mwaikimba na beki Said Morad ambaye Yanga inamuwania kwa udi na uvumba.
SWACOTZ FORUM lilipomtafuta Katibu Mkuu wa timu hiyo, Nassor Idrissa alisema, ni mapema kuzungumzia wachezaji wanaoachwa lakini itakapofika muda wake mambo yote yatawekwa hadharani.

No comments:

Post a Comment