EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Saturday, March 1, 2014

NDANDA YAWEKWA KITI MOTO MECHI NA TESEMA

NA KASSIM NGUMBI:...Mtwara

Afisa michezo Mtwara Vijijini Nicolous mmuya  akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao

Uongozi wa kamati ndogo ya saidia ndanda ishinde unaoongozwa na Afisa michezo wa mkoa wa mtwara Ndg Rogers Bahati akishirikiana na afisa michezo wa manispaa ya mtwara ,ikindani Bi:Yusura Kayombo Pamoja na afisa wa michezo wa halmashauri ya Mtwara vijijini Ndg Nicolous MMuya jana wamewakutanisha viongozi na wachezaji wa timu ya ndanda na wazee 
maarufu pamoja na wale waliowahi kushiriki michezo enzi za ujana wao.
mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu mkoani mtwara MTWAREF
 katika chakula cha pamoja cha jiono ili wazee hao waweze kuwapa vijana wao na mbinu za kimichezo ambazo zitswafanya waweze kushinda katika mechi zao zilizosalia. katika ghafla hiyo iliyofanyika jana kuanzia saa moja usiku mpaka majira ya saa nne za usiku katika hoteli ya Pensura mtwara mjini ambayo pia ilihuzuriwa na viongozi wengine wa michezo akiwemo mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu mkoani mtwara Ndg Hashim Kambi.
MOJA KATI YA WAZEE WALIOHUDHULIA AKIZUNGUMZA NA WACHEZAJI HAWAPO PICHANI
wazee mbalimbali akiwamo mzee dogoa walizungumza kwa kuwapa mifano vijana hao ya namna ya kutafuta ushindi katika mechi zao hususani kwa kipindi hiki cha lala salama lakini pia kwa upande wake mwenyekiti wa Mtwarefa NDG Kambi yeye aliwaahidi vijana wa ndanda kuwa chama cha soka mkoani mtwara kipo nyuma yao nakuwataka wasiwe na hofu yeyote.
BAADHI YA WACHEZAJI WA TIM YA NDANDA FC
hivyo wajiamini kwa kila wakifanyacho wakati aliyekuwa mgeni rasmi ofisa michezo wa mkoa.

naye pia alieleza namna serikali kupitia ofisi ya mkuu wa mkoa ilivyojipanga kuisaidia ndanda na kwamba wao wasikate tamaa wakaze buti.awali ndanda ilisaidiwa chini ya kamati inayoongozwa na mkuu wa wilaya ya mtwara MH:Willmani Kapenjama Ndile na baada ya hapo ingawa kamati hiyo bado inaendeleza msaada wake lakini sasa watu wengi wa mtwara wameonekana kuguswa na hilo ambapo kila mmoja sasa amekuwa ni sehemu ya mchango kwa timu hiyo ili kuhakikisha inapanda daraja,jumamosi iliyopita ya february 22 ndanda ilicheza na afrikan lyion klatika nuwanja wa nangwanda mjini mtwara na ndandsa ikaibuka kidedea kwa ushindi wa bao moja kwa nunge na jumamosi hii yaani kesho march mosi ndanda itakua uwanjani tena nangwanda kukipiga na Tesema fc mchezo ambao utaanza majira ya saa kumi kamili nza jioni kwa saa za afrika mashariki.
KILA LA KHERI NDANDA HAPO KESHO.

No comments:

Post a Comment