EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Wednesday, January 22, 2014

TUkio kubwa la kusikitisha lililotokea siku ya jana mkoani mtwara na kusababisha majeruhi ya wana funzi 51 bado limeendelea kuiweka mtwara katika majinzi hii leo

NA: KASSIM NGUMBI

WANAFUNZI watano wanaosoma vidato tofauti katika shule ya sekondari ya Mustafa Sabodo, wamefariki dunia mapema jana, kufuatia kukanyangwa na gari ndogo aina ya Mercedez Benz, wakati wakiwa katika mchakamchaka wa asubuhi katika barabara kuu ya Mtwara kwenda Dar es salaam, maeneo ya Msijute. 

            

 Kamanda wa Polisi mkoa wa Mtwara, Zelothe Stephine, akiwa ndandi ya  wodi namba moja katika Hospitali ya mkoa ya Ligula, alipokwenda kuwaona majeruhi wa ajali  ya  wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mustafa Sabodo, iliyotokea leo katika barabara ya Mtwara Lindi wakati wanafunzi wa shule hiyo wakikimbia mchakamchaka asubuhi. Kushoto Kaimu Katibu tawala wa Mkoa Smythies Pangisa. Katika ajali hiyo iliyohusisha gari ndogo aina ya Masdz Benzi lenye namba za usajili T174 AEB imesababisha vifo vya wanafunzi wanne na wengine 47 kujeruhiwa

Kwa mujibu wa taarifa ilizozifikia chumba cha habari cha Pride Fm Radio, kutoka kwa kamanda wa polisi wa mkoa wa Mtwara ACP Zelothe Stephen zimetaja wanafunzi waliofariki katika tukio hilo kuwa ni pamoja na Hilda Mathias Nguli, Khailat Mohammed Saidi, Mwanahamisi Hassan Mohammed, Nasma Salum Mkunja na Farida Ally.


Amesema kuwa mwanafunzi mmoja alifariki papo hapo eneo la tukio baada ya kukanyagwa kabisa na gari hilo, wawili walifariki njiani na mmoja alifariki baada ya kufikishwa katika hospitali ya mkoa ya ligula kwa matibabu zaidi.

 Mmoja wa majeruhi akipelekwa wodini baada ya kupokewa katika hospitali hiyo

Kamanda Zelothe amesema kuwa jumla ya wanafunzi 51 walikutwa na mkasa huo, ambapo kati ya hao wanafunzi 46 wamejeruhiwa, huku wanafunzi 28 wakitibiwa na kuruhusiwa kurudi makwao, ambapo wanafunzi wengine bado wamelazwa wakiendelea na matibabu.




                            Kamanda wa Polisi, Zelothe Steven akizungumzia ajali hiyo

Naye Mganga Mfawidhi wa hospitali ya mkoa ya Ligula Mohammed Gwao amesema kuwa wanafunzi wawili Joel Simon miaka (13) na Sabaha Badilu miaka (13), wamehamishiwa katika hospitali ya Nyangao kwa matibabu zaidi ya mifupa, na hivyo kubaki na majeruhi 17 wanaondelea kupokea matibabu katika hospitali hiyo ya Ligula.


Kamanda Zelote akikagua gari lililohusika katika ajali hiyo 
 Kamanda huyo amesema kuwa dereva wa gari hilo aina ya Mercedez Benzi Station Wagon, lenye namba za usajili T 174 AED Mbaraka Bakari Mgwegwe mfanyabiashara mwenye umri wa miaka (50) anashikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano na uchunguzi kamili wa ajali hiyo.

No comments:

Post a Comment