MENEJA wa klabu ya
Chelsea, Jose Mourinho amekiri kufurahishwa na kumsajili kwa mara
nyingine Nemanja Matic na kumsifia kuwa mmoja wa viungo bora kabisa hivi
sasa. Nyota huyo wa kimataifa wa Serbia aliondoka Chelsea na kuhamia
Benfica mwaka 2011 ikiwa kama sehemu ya Chelsea kumsajili David Luiz
lakini kiungo huyo amerejea tena darajani kwa ada ya euro milioni
25. Ujio wa kiungo huyo umekuwa faraja kwa Mourinho ambaye amedai kuwa
atakuwa sehemu muhimu katika kikosi chake ambacho kinafuukuzia taji la
Ligi Kuu na Ulaya. Matic amerudi Chelsea kuchuana kutafuta namba katika
kikosi cha kwanza na kina John Obi Mikael, Frank Lampard, Ramires na
Michael Essien na ana uhakika kuwa safari hii anaweza kupata namba
katika kikosi hicho.
No comments:
Post a Comment