KENYA YATUMA VIKOSI MAALUM KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA
RAIS UHURU KENYATA WA KENYA
Serikali ya Kenya imetuma vikosi maalum
vitatu, kupambana na hali ya kuongezeka kwa matumizi ya dawa za kulevya, na
uwepo wa silaha haramu, vinavyoathiri vijana wasiokuwa na ajira katika sehemu
ya kaskazini mwa Kenya. Hatua ya serikali inatokana na wasiwasi
waliouonesha wazee wa kikabila katika sehemu ya kaskazini mwa Kenya, waliosema
matatizo hayo yanachangia kuvuruga usalama katika sehemu ya kaskazini mwa
Kenya.
Katika miezi ya hivi karibuni kumekuwa na
tatizo la kuongezeka kwa uhalifu katika eneo la Bungoma, ambako watu 30
waliuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa, katika eneo la Trans Nzoia watu 15
waliuawa, ikiwa ni pamoja na polisi watatu.Watu hao waliuawa na majambazi walionunua
silaha haramu kutoka Uganda.Tatizo la umasikini na ukosefu wa ajira
yanachangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la uhalifu katika sehemu mbalimbali za
Kenya.
No comments:
Post a Comment