EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Sunday, July 28, 2013

WATANZANIA MADAWA YA KULEVYA YANATUHARIBIA SIFA YA NCHI MWINGINE AKAMATWA TENA KULEVYA HONG KONG

  


 Mtu mmoja jana alisema sasa hivi wasafiri watokao Tanzania wanakaguliwa kwa makini zaidi ya ilivyokuwa hapo awali kutokana na matukio ya kukamatwa na dawa za kulevya! Hii ni sifa mbaya mno kwa raia na Taifa zima!Iliyopachikwa hapo chini ni taarifa kutoka kwenye tovuti ya Serikali ya Hong Kong ya Julai 26, 2013 Hong Kong Customs yesterday (July 25) detected three drug trafficking cases, with seizures totally valued at $4.78 million, in the department's escalated anti-narcotics efforts to combat drugs.     Customs officers at the Hong Kong International Airport (HKIA) intercepted a 26-year-old incoming...

HAUSIBOI ALIYEMLAWITI BINTI WA MIAKA MINNE AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA JELA HUKO MPANDA


Mahakama  ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi imemhukumu kijana, Baraka  Juma (22) mkazi wa kijiji cha Nkungwi  wilayani humo, kifungo cha maisha jela  baada ya kupatikana  na hatia  ya  kosa la kumlawiti mtoto wa kike mwenye umri  wa  miaka minne  baada  ya kumhadaa na  kumlewesha bia. Akisoma  hukumu  hiyo  juzi, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Chiganga Tengwa  alisema ameridhishwa  na  ushahidi  pasipo kutia shaka uliotolewa mahakamani hapo na upande zote  mbili za mashitaka na utetezi.  “Nimelazimika...

MBUNGE NASSARI ASOTA POLISI KWA MADAI YA KUMPIGA KADA WA CCM


Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari jana alishikiliwa na jeshi la polisi mkoani Arusha kwa saa tatu na nusu kwa tuhuma za kumshambulia kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Hussein Warsama siku ya uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Makuyuni, wilayani Monduli. Nassari aliyefika Kituo Kikuu cha Polisi Arusha saa 2:30 asubuhi jana ili kuitikia wito wa kutakiwa kuripoti kituoni hapo, alinusurika kuswekwa mahabusu baada ya kujidhamini mwenyewe majira ya saa saa 6:02 mchana na hivyo kuachiwa kwa dhamana. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai mkoani Arusha (RCO), Nassari anadaiwa kumshambulia Warsama...

VIDEO YA MWANACHUO AKIKATA MAUNO NUSU UCHI....


  Katika hali isiyo ya kawaida, mwanafunzi mmoja wa kike wa chuo kikuu maarufu hapa nchini ametoa kali ya mwaka baada ya kuamua kupiga chini kitabu na kuanza kukata mauno huku akiwa na kikanga kimoja kiuoni na sehemu kubwa ya mwili wake ikiwa wazi hasa matiti....Video iko hapo chini: <<VIDEO  IKO  HAPA>>...

PROGRAM YA AJIRA KWA VIJANA WALIOHITIMU VYUO VIKUU NCHINI....


PROGRAMU YA AJIRA Programu hii itatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na vyuo vya elimu ya juu nchini,Taasisi za fedha na wabia wa maendeleo.Kwa kuanzia utekelezaji wake utaanza kwa kuendeleza programu ya mfano iliyoanzishwa na Idara ya kilimo, uchumi na Biashara katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (DAEA-SUA) na hatimaye kuwafikia wahitimu wa vyuo vingine vya elimu ya juu katika kipindi husika. Kwa kuanzia serikali imekubaliana na Benki ya CRDB kuanza utoaji wa mikopo kwa vijana mara  utekelezaji wa programu utakapoanza. Kwa kuwa kasi ya wanaojiunga elimu ya juu nchini imeongezeka wastani wa (48% kwa mwaka) na Wizara imeona...

USABATO WADAIWA KUKIANGAMIZA CHUO CHA AURUSHA (UoA)

Haya  ni  malalamiko ya  mdau anayesimulia  jinsi  USABATO unavyokiangamiza  chuo cha Ausha... Katika  maelezo  yake  aliyoyatoa  mzalendo forum, mdau  huo  anaripoti  kuwa  bila  kuwa  msabato  huwezi  kuajiriwa  chuoni  hapo, bila  kuwa  msabato  huwezi  kushinya  uongozi  wowote  wa  wanafunzi..... Je  kuna  ukweli  wowote??? HUU  NDO  UJUMBE  WAKE <<USABATO  WA  CHUO  CHA  ARUSHA>&...





VIDEO: ANGALIA NAMNA BAYERN MUNICH WALIVYOPIGWA 4-2 NA DORTMUND KATIKA MECHI YA KUFUNGUA MSIMU WA BUNDESLIGA

Dortmund imeifunga Bayern Munich 4-2 katika mchezo wa Supercup uliochezwa leo.
[FutbolHD.ru] Borussia Dortmund 4-2 Bayern... by all-goals
 

HIVI NDIVYO TAIFA STARS ILIVYONYOLEWA NA UGANDA THE CRANES NA KUSHINDA KWENDA CHAN

Wachezaji wa timu ya taifa 'Taifa Stars' na Uganda Cranes wakiingia uwanjani tayari kwa kuanza mechi yao ya kufuzu kucheza Chan iliyofanyika kwenye uwanja wa Mandela, Namboole mjini Kampala.


Kikosi cha timu ya taifa ya Uganda 'Uganda Cranes'


Mchezaji wa Taifa Stars Aggrey Morris (katikati) akiwania mpira huku akizongwa na mabeki wa Uganda Cranes.Taifa Stars inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.

Amri Kiemba akipongezwa na Mrisho Ngasa/ Aboubakar Salum 'Sure Boy' baada ya kushinda bao la kusawazisha dhidi ya Uganda Cranes



Washabiki wa Taifa Stars wakishangilia goli la kusawazisha..

Kiemba







HATIMAYE TAIFA STARS WATOLEWA CHAN - WAPIGWA 3-1 NA UGANDA THE CRANES


Tanzania (Taifa Stars) imeshindwa kufuzu Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) kwa mara ya pili mfululizo baada ya leo (Julai 27 mwaka huu) kufungwa mabao 3-1 na Uganda Cranes, hivyo kutolewa kwa jumla ya mabao 4-1.
Stars ambayo ilicheza fainali za kwanza zilizofanyika Ivory Coast mwaka 2009 ilimaliza kipindi cha kwanza katika mechi hiyo iliyochezwa Uwanja wa Taifa wa Mandela ulioko Namboole nje kidogo ya Kampala ikiwa sare ya bao 1-1.
Wenyeji ndiyo walioanza kufunga bao dakika ya saba katika mechi hiyo iliyochezeshwa na Kanoso Abdoul Ohabee kutoka Madagascar. Frank Kalanda alifunga bao hilo akimalizia mpira uliopigwa ndani ya eneo la hatari la Tanzania.
Bao hilo halikuonekana kuichangaza Taifa Stars, kwani ilitulia na kufanikiwa kusawazisha dakika ya 18 mfungaji akiwa Amri Kiemba kutokana na pasi nzuri ya Mrisho Ngasa kwenye kona ya eneo la mita 18.
Dakika ya 32 nusura Taifa Stars ipate bao, lakini mkwaju maridadi wa Mrisho Ngasa ambao tayari ulikuwa umempira kipa HAmza Muwonge uligonga mwamba kabla ya kuokolewa na mabeki wa Uganda Cranes.
Mabao mengine ya Uganda Cranes yalifungwa dakika ya 48 kupitia kwa Brian Majwega na lingine dakika ya 63 mfungaji akiwa tenda Kalanda kutokana na makosa ya Salum Abubakar kupokonywa mpira wakati akiwa katika nafasi nzuri ya kutoa pasi kwa mwenzake.
Kocha Kim Poulsen alifanya mabadiliko dakika ya 43 kwa kumuingiza Simon Msuva badala ya Frank Domayo aliyeumia, na dakika ya 78 akawaingiza kwa mpigo Haruni Chanongo na Vincent Barnabas badala ya David Luhende na John Bocco. Hata hivyo mabadiliko hayo hayakubadili matokeo ya mchezo.
Kikosi cha Stars kilipangwa hivi; Juma Kaseja, Erasto Nyoni, David Luhende/Vincent Barnabas, Aggrey Morris, Kelvin Yondani, Athuman Idd, Frank Domayo/Simon Msuva, Salum Abubakar, John Bocco/Haruni Chanongo, Amri Kiemba na Mrisho Ngasa.
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itarejea nyumbani kesho (Julai 28 mwaka huu) saa 4 usiku kwa ndege ya PrecisionAir.

No comments:

Post a Comment