EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Sunday, July 21, 2013

ASKARI DAR WAVAMIA MKUTANO WA CHADEMA WAPIGA MABOMU TAHARUKI YATANDA

VITUKO na matukio ya hatari kwenye mikutano ya CHADEMA vimeendelea kushika kasi.

 Mh John Mnyika akihutubia wakazi wa Ubungo


Jana Mbunge wa Ubungo, John Mnyika alinusurika kupigwa na bomu la machozi lililorushwa na polisi waliokuwa wakizuia kufanyika mkutano ulioitishwa na chama hicho.
Tukio hilo lilitokea katika eneo la Mabibo kwenye viwanja vya Sahara ambapo bomu hilo lilimpata mtu aliyekuwa karibu na Mnyika anayeitwa Thomas Jerome, aliyejeruhiwa sehemu ya paja.
Baada ya kurushwa kwa bomu hilo, polisi walitaka kumchukua majeruhi huyo ili wamweke kwenye gari lao apelekwe hospitalini, lakini Mnyika aliwaelekeza wafuasi wa CHADEMA kumchukua kwa madai kitendo kilichofanywa na askari hao kililenga kuficha ushahidi wa jambo hilo.
Polisi waliokuwemo eneo la tukio waliamua kukubaliana na matakwa ya wafuasi wa CHADEMA waliomchukua Jerome na kumpeleka hospitali ambako hali yake inadaiwa inaendelea vizuri.
Akielezea hali ilivyokuwa akiwa katika mkutano mwingine uliofanyika Ubungo, Mnyika alisema polisi walifika katika viwanja vya Sahara wakiwa na magari matatu kwa lengo la kutawanya wafuasi wa CHADEMA wasifanye mkutano wakidai haukuwa na baraka za jeshi hilo.

Mnyika alisema polisi hao walisema sababu ya kuuzuia mkutano huo ni uwepo wa ziara ya Makamu wa Rais katika Wilaya ya Kinondoni, hivyo walikuwa wameelekeza nguvu zao katika ziara hiyo, kwamba hawakuwa na uwezo wa kuulinda mkutano wa CHADEMA.
“Nikiwa nimejiandaa kupanda jukwaani ndiyo polisi walikuja kusema tuache tusifanye mkutano, nilisogea karibu na gari kumlalamikia ofisa wa polisi kwani kitendo cha kuahirisha mkutano kwa barua waliyoileta saa sita mchana siku ya mkutano wakati sisi tuliwapa taarifa siku nne zilizopita ilikuwa sio haki.
“Nilimwambia ofisa huyo wa polisi kuwa nilikuwa najadiliana kwa simu na viongozi wakuu wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam na Inspekta Jenerali wa Polisi Said Mwema kumlaumu kutumika vibaya kwa Jeshi la Polisi.
“Nilipokuwa bado najibizana naye bila fujo zozote, bomu lilirushwa kutoka ndani ya gari ya polisi na kupita karibu na mimi likamjeruhi mtu aliyekuwa karibu yangu, ki ukweli nimeshangazwa sana na matumizi mabaya ya silaha za moto,” alisema.
Aliongeza kuwa katika purukushani zilizotokea baada ya bomu kupigwa, alipoteza nyaraka mbalimbali alizokuwa amebeba kama ushahidi kuwaonyesha wafuasi wa chama hicho hasa jinsi serikali ya CCM na wabunge wake walivyopitisha kodi ya huduma za simu, na kodi ya laini za simu.
Slaa anena
Aidha katika mkutano huo ambao awali ulitangazwa kuwa ungehutubiwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, haukuweza kuhutubiwa naye kwa kile alichosema kuwa watu wake wa usalama walimwambia mapema hali si salama kwenye mkutano huo.
“Nilipata taarifa kutoka vyanzo vyangu kuwa polisi walikuwa na mpango wa kuleta fujo, hivyo nikaona kwa kuwa wanatuwinda nisingeenda kuhutubia, pengine bomu lililomkosa Mnyika lilikusudiwa kwangu au kwa mwingine,” alisema Dk. Slaa alipozungumza na gazeti hili kwa njia ya simu baada ya kutoonekana mkutanoni.

Bonyeza Read More Kuendelea

CCM waihofia CHADEMA 2015

MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa CCM, Sophia Simba amesema anahofia CHADEMA wanaweza kunyakua Jimbo la Babati Mjini au Vijijini.
Simba alisema CHADEMA inaweza kufanya hivyo iwapo viongozi na wanachama wa CCM watabweteka na kutowahamasisha watu wengi kujiunga na chama hicho tawala.
Kiongozi huyo alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na viongozi wa CCM Mkoa wa Manyara kabla ya kuanza ziara yake ya siku tatu wilayani Babati.
Simba alisema viongozi na wanachama wa CHADEMA wanajituma katika kufanya kazi zao kichama, hivyo ni vema CCM wakaacha mazoea ya kuhamasisha kila chaguzi zinapokaribia.
“Mnawaona wenzetu wa CHADEMA wanavyohangaika huko kwa wananchi kutafuta wapiga kura kwa nguvu, na hii inaleta wasiwasi kwamba ikifika mwaka 2015 wanaweza hata kunyakua Jimbo hapa Babati, aidha Mjini au Vijijini,” alisisitiza Mwenyekiti huyo.
Alisema ili kuifanya CCM iwe imara ni lazima viongozi wa jumuiya zote ikiwemo ya vijana kuhamasisha watu kujiunga.
Simba alisema uhamasishaji huo ikibidi uendane na wanachama hao kutotoa ada za uanachama ili kuwavutia wengi zaidi.
“Tafuteni wanachama kwa nguvu zenu zote, ikibidi hata msiwalazimishe kulipa ada za chama na kuwaita wanachama wafu kwani mkiwaita wafu wataenda kwa wenzetu wa CHADEMA wanakochukuliwa bure,” alisema Simba.
Alisema miongoni mwa sababu zilizokifanya chama hicho kishindwe kwenye chaguzi ni kutowajibika ipasavyo katika uhamasishaji wa kutoa mwamko wa kisiasa kwa wanachama wake.
Simba alisema hali ni tofauti kwa wapinzani wao ambao kila kukicha wamekuwa wakihahangaika kwa wananchi huku wakifanya mikutano mbalimbali ya kuwarubuni kisiasa.
Alisisitiza kuwa viongozi wasiwachukulie kimzaha mzaha wapinzani wao kwani wanafanya mikakati na maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
“Tuache kufanya kazi kwa mazoea, tunapofikiria sisi ni chama tawala na kubweteka tukisubiri wakati wa kampeni tutaumia, wenzetu mnawaona,” alisema.

CCM waihofia CHADEMA 2015

MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa CCM, Sophia Simba amesema anahofia CHADEMA wanaweza kunyakua Jimbo la Babati Mjini au Vijijini.
Simba alisema CHADEMA inaweza kufanya hivyo iwapo viongozi na wanachama wa CCM watabweteka na kutowahamasisha watu wengi kujiunga na chama hicho tawala.
Kiongozi huyo alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na viongozi wa CCM Mkoa wa Manyara kabla ya kuanza ziara yake ya siku tatu wilayani Babati.
Simba alisema viongozi na wanachama wa CHADEMA wanajituma katika kufanya kazi zao kichama, hivyo ni vema CCM wakaacha mazoea ya kuhamasisha kila chaguzi zinapokaribia.
“Mnawaona wenzetu wa CHADEMA wanavyohangaika huko kwa wananchi kutafuta wapiga kura kwa nguvu, na hii inaleta wasiwasi kwamba ikifika mwaka 2015 wanaweza hata kunyakua Jimbo hapa Babati, aidha Mjini au Vijijini,” alisisitiza Mwenyekiti huyo.
Alisema ili kuifanya CCM iwe imara ni lazima viongozi wa jumuiya zote ikiwemo ya vijana kuhamasisha watu kujiunga.
Simba alisema uhamasishaji huo ikibidi uendane na wanachama hao kutotoa ada za uanachama ili kuwavutia wengi zaidi.
“Tafuteni wanachama kwa nguvu zenu zote, ikibidi hata msiwalazimishe kulipa ada za chama na kuwaita wanachama wafu kwani mkiwaita wafu wataenda kwa wenzetu wa CHADEMA wanakochukuliwa bure,” alisema Simba.
Alisema miongoni mwa sababu zilizokifanya chama hicho kishindwe kwenye chaguzi ni kutowajibika ipasavyo katika uhamasishaji wa kutoa mwamko wa kisiasa kwa wanachama wake.
Simba alisema hali ni tofauti kwa wapinzani wao ambao kila kukicha wamekuwa wakihahangaika kwa wananchi huku wakifanya mikutano mbalimbali ya kuwarubuni kisiasa.
Alisisitiza kuwa viongozi wasiwachukulie kimzaha mzaha wapinzani wao kwani wanafanya mikakati na maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
“Tuache kufanya kazi kwa mazoea, tunapofikiria sisi ni chama tawala na kubweteka tukisubiri wakati wa kampeni tutaumia, wenzetu mnawaona,” alisema.

BAVICHA mwenyeji mkutano wa IYD

BARAZA la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA), linatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Bodi ya Umoja wa Vyama vya Demokrasia Duniani (IYDU), utakaofanyika kuanzia Julai 25 hadi 30, jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini mwishoni mwa wiki, Katibu Mkuu wa BAVICHA, Deogratias Munishi, alisema mkutano huo utafunguliwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa na utafungwa na Mwenyekiti wa Taifa, Freeman Mbowe.
Alisema IYDU inayoundwa na mataifa 81, katika historia Tanzania inakuwa nchi ya kwanza kuwa mwenyeji wa mkutano huo kwa nchi za Afrika zilizoko Kusini mwa Jangwa la Sahara.
“Hii ni heshima ya pekee kwa BAVICHA, CHADEMA, Vijana wa Tanzania na taifa zima kwa ujumla,” alisema.
Alisema baraza hilo litatumia mkutano huo kuwapatia washiriki fursa ya kujua kama demokrasia na mfumo wa vyama vingi nchini, tasnia ya habari na nafasi yake katika maendeleo ya demokrasia, uzoefu wa kujenga jamii za kidemokrasia kupitia mabadiliko ya katiba.
Munishi alisema masuala mengine watakayojadili ni uwezeshaji na hali ya kiuchumi ya vijana wa Afrika kwa mtazamo wa sera za CHADEMA na fursa na changamoto kwa vijana wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Aidha, alisema mkutano huo utakuwa ni fursa ya kuitangaza Tanzania katika sekta ya utalii kwa kuwa wanaamini kama taifa bado hawajafanikiwa kujitangaza vilivyo kupitia nyanja hiyo.
Alisema watoa mada katika mkutano huo watakuwa Mabere Marando (mwanasiasa mwandamizi na wakili wa kujitegemea), Jaji Thomas Mihayo (Jaji Mstaafu, Mwenyekiti wa Tume ya Maadili ya Baraza la Habari Tanzania), Wakili Francis Stolla (Rais wa Chama cha Mawakili Tanzania), John Mnyika (Makamu wa Rais mstaafu wa IYDU) na Jenerali Ulimwengu (Mwandishi mwandamizi).
Alisema ujumbe wa IYDU utapata fursa ya kuwa na mazungumzo na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Jumuiya ya Ulaya nchini na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini (LHRC). Pia ujumbe huo utakutana na Spika wa Bunge la Tanzania na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

No comments:

Post a Comment