EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Thursday, May 23, 2013

Rais Obama kuzuru Afrika; kukaa Tanzania siku mbili

Rais Obama kuzuru Afrika; kukaa Tanzania siku mbili


Rais wa Marekani Barack Obama anatarajiwa kuzuru Senegal, Afrika Kusini na Tanzania mwezi Juni. Hii ni kwa mujibu wa taarifa kutoka ikulu ya White house.
Rais Obama atakutana na watunga sheria na wafanyabiashara pamoja na viongozi wa asasi za kijamii.
Alizuru Ghana mwaka 2009 .Ziara ya Obama itaanza tarehe 26 Juni hadi 3 Julai na itakuwa ziara yake ya pili Kusini mwa jagwa la Sahara akiwa rais wa Marekani.

Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton na mwenzake George W Bush, wote walizuru Afrika wakati wa muhula wao wa pili wa utawala.
Clinton alizuru nchi sita wakati Bush akizuru nchi tano.
''Rais atatilia mkazo uhusiano kati ya Marekani na baadhi ya nchi za kiafrika ambazo zinakuwa ikiwemo maswala kama ukuwaji wa uchumi, uekezaji na biashara pamoja na kukuza taasisi za kidemokrasia na kuendelea kukuza viongozi wa kizazi kijacho Afrika,'' ilinukuu taarifa kutoka ikulu ya White House.
Soma zaidi

No comments:

Post a Comment