EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Thursday, April 3, 2014

KAMANDA WA POLISI MTWARA AWAPA SOMO BODABODA BAADA YA KUTOKEA KWA MAANDAMANO MAKUBWA YA KUPINGA UVAAJI WA KOFIA NGUMU YAANI HELMENT


NA : MWANDISHI WETU
Kufuatia maandamano ya waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda wanaofanya shughuli zao katika manispaa ya Mtwara Mikindani Kamanda wa polisi mkoani Mtwara ACP Zelothe Steven amewataka kutii sheria zilizowekwa na nchi.
Kamanda Zelothe ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake na kueleza kuwa jeshi la polisi halitosita kumchukulia hatua mtu yeyote atakayevunja sheria kwa kuwa ni wajibu wa kila mwananchi kutii sheria.
Amesema kutokana na kitendo cha kufunga baadhi ya barabara na maandamano yaliyofanywa na bodaboda hao hapo jana, ambayo yalisababisha kero kwa wananchi wengine uamuzi wa jeshi polisi kutuliza ghasia ulikuwa ni sahihi kwa kuwa ulikuwa ni uvunjaji wa sheria.
Katika Ghasia hizo za jana jeshi hilo limekamata jumla ya pikipiki 27 zilizotelekezwa na waendeshaji wa pikipiki hizo ambao walikimbia na watu tisa wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi.
Aidha jeshi hilo limewakamata majangili watatu katika kijiji cha Masuguru wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara wakiwa katika maandalizi ya kwenda katika hifadhi ya Lukwika Lumesule kutekeleza azma ya kutenda uhalifu.
Watuhumiwa hao walikamatwa silaha mbalimbali ambazo ni Bunduki aina ya Rifle 458 yenye namba 083972, Risasi 25 za 458, upinde mmoja na mishale minne, mapanga matatu, silaha nyingine ni visu viwili, tupa mbili, oil chafu robo lita na vyakula aina mbalimbali na jeshi hilo linaendelea na msako wa watuhumiwa wengine ambao wamekimbia.
 Pia jeshi hilo limemkamata Mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Julius Simon mwenye umri wa miaka 32 katika kijiji cha Lukula Kata ya masuguru wilayani Nanyumbu akiwa na meno 35 ya Tembo yenye uzito wa kilogramu 81.8 ambayo thamani yake ni shilingi milioni 451,440,00  swa na tembo kumi na nane waliouwawa.
       

No comments:

Post a Comment