Mkuu wa mkoa Lindi Ludovick Mwananzila |
Shule za Msingi na Sekondari, mkoani Lindi, zinakabiliwa
na upungufu mkubwa wa madawati, yapatayo 32,476 jambo ambalo linawasababishia
idadi kubwa ya wananfunzi kulazimika kusoma wakiwa wameketi sakafuni.
Mkuu wa mkoa Lindi Ludovick Mwananzila ameyabainisha hayo wakati alipokuwa
akipokea msaada wa madawati 110 yenye thamani ya Shilingi milioni 20 kutoka
mamlaka ya usimamizi wa Bandari Mtwara (TPA).
Akizungumza na wananchi katika hafla ya kupokea msaada huo, mkuu huyo wa mkoa
amesema mahitaji ya madawati kwa mkoa wake ni 68,907 wakati yaliyopo ni 36,431
tu, na kufanya upungufu wa madawati 32,476.
Mwananzila amesema kwa upande wa Shule za msingi kuna upungufu wa madawati
21,988 wakati shule za Sekondari nazo zinakabiliwa na
upungufu wa madawati 10,488.
upungufu wa madawati 10,488.
Amesema Halmashauri ya Lindi vijijini inaoongoza kwa
upungufu wa madawati (6,427), ikifuatiwa na Nachingwea yenye madawati (8,584) na kufanya upungufu (6,904) sawa na asilimia 40.58, Ruangwa mahitaji ni 11,802 lakini yaliyopo ni 9,211 na kufanya pungufu 2,591 sawa na asilimia 31.91.
upungufu wa madawati (6,427), ikifuatiwa na Nachingwea yenye madawati (8,584) na kufanya upungufu (6,904) sawa na asilimia 40.58, Ruangwa mahitaji ni 11,802 lakini yaliyopo ni 9,211 na kufanya pungufu 2,591 sawa na asilimia 31.91.
Mwananzila amesema wilaya ya Kilwa mahitaji ya madawati ni,10,605, yaliyopo
ni (9,026) na kufanya pungufu (1,579) sawa na asilimia 14.89, Liwale ina upungufu
wa madawati (1,984) wakati mahitaji ni 7,799 huku yaliyopo 5,815, Manispaa ya Lindi,
inayo madawati 3,677 wakati mahitaji ni 6,180 na kufanya upungufu wa madawati 2,503.
MWISHO.
Chanzo, Mwanja Ibadi mwananchi.
No comments:
Post a Comment