![]() |
| MKUU WA WILAYA YA MTWARA MH: WILLMAN NDILE KWA MBALI AKIZUNGUMZA NA WATENDAJI WA KATA WAKATI WA KIKAO. |
NA KASSIM NGUMBI ……..Mtwara
Hayo yalisemwa na mkuu wa wilaya ya Mtwara MH: Willman Kapenjama Ndile Katika kikao
kilichofanyika jana ndani ya ukumbi wa boma kwenye ofisi ya mkuu wa mkoa mtwara
ambacho kilihusisha maafisa watendaji wa mitaa toka manispaa ya Mtwara
Mikindani,wakuu wa idara wa manispaa akiwemo Daktari wa manispaa, Mwanasheria
wa Manispaa Afisa Afya na Afisa Utumishi pamoja na watu wanaotoka sektwa za
ulinzi na usalama kwa maana ya ofisi ya kamanda wa polisi wa mkoa na ofisi ya
jeshi la magereza la mkoa na mkurugenzi wa manispaa ya Mtwara Mikindani na
kuchukua takribani masaa mawili na nusu kuanzi saa nane za mchana mpaka saa
kumi alaasiri.
Kikao hicho kilikuwa na lengo la kuzungumzia mambo yapatayo
matatu ambapo la kwanza lilikuwa ni swala nyeti la usafi wa mji,lapili ni swala
la uwepo wa mifugo kupitiliza katikati ya mji, na swala la tatu ni swala la
upigaji muziki kupita kiasi katika nyakati za usiku maeneo ya baa zilizopo
katikati ya makazi ya watu.
Awali katika
maelezo yake kabla ya kuanza kuzungumzia haya mh dc alieleza mafanikio yaliyopatikana kutokana na
tamko lake alilokalitoa wiki mbili zilizopita la kuwataka wazazi wote ambao
bado hawajawapeleka watoto wao ambao wamefaulu kujiunga na kidato cha kwanza
katika shule zao na kutoa agizo la kwamba wasipofanya hivyo basi watachukuliwa
hatua kali za kisheria. Awali katika tamko lake hilo Ndile alitoa siku saba kwa
wazazi kutekeleza agizo hilo na wakati tamko hilo likitoka uwiano wa watoto
kwenda mashuleni kwa upande wa halmashauri ya mtwara vijijini ambayo ipo ndani
ya wilaya yake ni watoto watatu tu katiya kumi ndio waliokua wamepelekwa shule
huku saba wakisalia nyumbani bila sababu maalum na kwa upande wa manispaa ya
mtwara mikindani uwiano ulikuwa ni watoto saba kati ya kumi ndio waliojiunga na
kidato cha kwanza huku idadi kamili ya watoto waliotakiwa kuanza kidato cha
kwanza ikiwa ni 1090. Lakini mpaka kufikia jan adc ndile alisema kuwa watoto
1083 tayari wamekwishaanza masomo na watoto saba tu ndio wamesalia huku
akiahidi kuwa baada ya wiki moja nao watakua wamekwenda shuleni kwa muhula mpya
wa masomo ya sekondari katika hili alitoa pongezi kwa maafisa watendaji wa
kata,mitaa na viongozi wa serikali za vijiji pamoja na vyombo vya habari ambao
wao walikuwa ni wadau wakubwa katika kuhamasisha na kuhakikisha hili swala
linafanikiwa.![]() |
| BAADHI YA WAJUMBE WAKIWA KIKAONI |
MAMBO MATATU YA KIKAO CHA JANA
1.
SWALA LA
KUZAGAA KWA MIFUGO KATIKATI YA MJI……kuhusu hili mkuu wa wilaya alinukuu
baadhi ya taarifa alizopelekewa juu ya kuwepo kwa hali ya kuzagaa kwa ng’ombe,
mbwa na nguruwe katika maeneo mengi ya mitaa ya katikati ya mji ambapo mifugo
hii inasababisha kero kubw kwa wakazi wa maeneo husika , akianza na swala la ng’ombbe
MH: NDILE alisema kuwa yeye mwenyewe amekwishawahi kushuhudia makundi makubwa
ya ng’ombe wakikatiza katikatio ya mji na kutaka kusababisha ajali lakini pia
uwepo wa mifugo ya aina hiyo ndani ya mji ni uchafu hivyo amewataka watendaji
wa mitaa kuhakikisha wanakamata mifugo nhiyo bila kujali nani mmiliki kwa
kuzingatia sheria na kuwatoza faini ya shili elfu sitini.
Lakini katika maeneo haya ya mifugo mkuu wa
wilaya alizungumzia pia suala la nguruwe na mbwa akasema kuwa nguruwe wamekuwa
wakilalamikiwa na wananchi wengi kwa kutoa harufu mbaya katika makzi wanayoishi
na kusababisha uharibifu wa hari ya hewa lakini pia mpaka sas amekwishapokea
kesi za watu waliong’atwa na mbwa zipatzo ishirini hivyo hili nalo limekuwa
kero na akataka watendaji kuhakikisha wanafuata sheria ambayo inataka kila mfugaji
ndani ya mji asifuge zaisdi wa wanyama watatu na akasema kuwa iwapo wanyama
kwama mbwa wakiwa wengi na ni kero basi watendaji wanao uwezo wa kuandika
muhtasari wa kuamuru kuuawa kwa mbwa hao.
2.
MUZIKI
KUPITILIZA…….PIA katika maelezo yake alisema kuwa sheria hiyo inazuia tabia
ya kupiga muziki kupitiliza nyakati za usiku hasa katika mabaa na mikesha ya
sherehe mbalimbali kwani swala hilo pia ni kero kwa wananchi wengine na kwamba
mtu atakayehitaji kufanya biashara ya muziki basi ahakikishe anajenga ukumbi
wenye sound proof na hili pia mkuu huyo wa wilaya ametoa agizo kwa watendaji
hao wa kata kulisimamia huku akihusisha na nyumba za ibada ambazo zimekuwa
zikipiga vyombo vyao kwa sauti za juu sana bila kuzingatia eneo kanisa au
msikiti ilipo.
3.
USAFI WA
MAZINGIRA…….mwisho amewataka watendaji hao kutumia sheria walizokabidhiwa
jana kwa kuhakikisha kila eneo ndani ya mji na wilaya mzima linakua safi kwa
kufyeka majani na kusafisha mitaro ili kuufanya mji wa Mtwara uwe na mazingira
mazuri. Watendsaji wote ambao walihudhulia jana katika kikao hicho
wamekabidhiwa nakala za sheria ambapo wamepewa wiki moja kuzipitia na baada ya
hapo atatangaza amri ya utekerezaji way ale yote waliyokubaliana kupitia kikao
hicho.


No comments:
Post a Comment