EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Wednesday, June 19, 2013

POLISI MKOANI ARUSHA ,CHADEMA NGOMA NZITO ARUSHA WADAI WAKO TAYARI KUPOKEA USHAHID WAO,MBOWE NA WENZAKE WATAFUTWA KWA UDI NA UVUMBA LEMA AJIFICHA KWA MCHOMA NYAMA ....WAANDISHI WAAMBULIA KICHAPO

 

Wabunge wanne wa Chadema, Said Arfi (Mpanda Mjini), Tundu Lissu (Singida Mashariki), Mustapha Akunaay (Mbulu) na Joyce Mukya (Viti Maalumu) wamekamatwa wakituhumiwa kuhusika na mkusanyiko usio halali kwenye Uwanja wa Soweto jana. Mkuu wa Operesheni wa Polisi, Kamishna Paul Chagonja alisema jana kwamba pamoja na wabunge hao pia wamewakamata watu wapatao 60 kutokana na vurugu zilizozuka jana baada ya Polisi kuwatawanya kwenye uwanja huo waliokuwa wamekusanyika kuomboleza vifo vya watu watatu; Judith Moshi, Ramadhan Juma na Amir Ally waliofariki kwenye mlipuko wa bomu uliotokea kwenye uwanja huohuo, Jumamosi iliyopita. Mbali ya viongozi...
Related Posts Widget For Blogger with ThumbnailsBlogger Templates TUPE MAONI YAKO

NAPE , GODBLESS LEMA NA MBOWE WATAKIWA KUPELEKA ASHAHIDI WAO POLISI, VINGINEVYO SHERIA ITACHUKUA MKONDO WAKE

Jeshi la Polisi limetishia kuwakamata Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema na limesema litamhoji Katibu Mwenezi wa CCM, Nape Nnauye baada ya wanasiasa hao kudai kufahamu watu waliohusika na tukio la kurushwa bomu mwishoni mwa wiki iliyopita. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Arusha jana, Mkuu wa Operesheni wa Polisi, Kamishna Paul Chagonja aliwataka wanasiasa hao kuwasilisha ushahidi wa kile wanachofahamu kuhusu kulipuliwa kwa bomu hilo. Juzi, Mbowe akiwa na Lema, alisema wana ushahidi wa picha za video zikiwahusisha polisi na kulipuliwa kwa bomu...
TUPE MAONI YAKO

JESHI LA POLISI LINAWASHIKILIA WABUNGE 4 WA CHADEMA KWA KUSABABISHA VURUGU ARUSHA

Jeshi la polisi mkoani Arusha linawashikilia viongozi wanne wa CHADEMA na watu wengine huku likiendelea kuwatafuta wabunge wawili na watu wengine.Jeshi la Polisi limesema limewatua nguvuni watu hao kwa makosa ya kuhutubia mkutano haramu wakati wa kuwaaga marehemu waliopoteza maisha kwenye mlipuko wa bomu uliotokea katika eneo la Soweto jijini humo mwishoni mwa wiki.Makosa mengine ni wanayotuhumiwa kwayo ni kufunga barabara na kuwashambulia askari polisi.Amesema wataendelea kubaki korokoroni hadi uchunguzi utakapokamilika.Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas amewataja Wabunge wanaoshikiliwa ni pamoja na Tundu Lissu na Mustapha...
TUPE MAONI YAKO

SABABU ZA JESHI LA POLISI KUTUMIA NGUVU YA MABOMU JIJINI ARUSHA MUDA HUU

Jeshi la polisi limekipiga marufuku chama cha demokrasia na maendelo(CHADEMA)kufanya shughuli zozote za kuaga miili ya marehemu kwenye viwanja vya Soweto kwani zoezi la uchunguzi bado linaendelea kwenye viwanja hivyo . Akizungumza ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani Arusha, Liberatus Sabas amesema kutokana na uchunguzi unaoendelea wa tukio la bomu kwenye viwanja hivyo imeonelea kuwa si busara kuweka mkusanyiko wa watu kwani kutaharibu upelelezi. Kamanda Sabas amedai  kuwa  jeshi la polisi  liliwataka viongozi wa chama hicho kuwaeleza wafuasi wao mahali sahihi watakapoweza kufanyia shughuli hiyo lakini...
TUPE MAONI YAKO

BREAKING NEWS: ARUSHA KWACHAFUKA TENA.....MABOMU YA MACHOZI YATUMIKA KUWATAWANYA WANANCHI

  Hali kutoka mkoani si nzuri...mabomu ya machozi yanapigwa  kuwatawanya  wananchi  waliojitokeza  kuiaga  miili ya  wananchi  waliofariki katika mlipuko wa bomu... Hivi sasa polisi wanapiga mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa CHADEMA waliofurika katika uwanja wa Soweto Mjini Arusha ulipotokea mlipuko wa bomu Jumamosi kuomboleza ambapo polisi inasema mkusanyiko huo si halali Taarifa toka mkoani humo zinadai kuwa gari la mh. Lissu liteketezwa vibaya kwa bom...
TUPE MAONI YAKO

MBUNGE ATAKA KISWAHILI KITUMIKA HADI VYUO VIKUU

MBUNGE wa Karagwe, Gosbert Blandes (CCM), amehoji lini serikali itapitisha Kiswahili kitumike kuanzia Shule za Msingi hadi Vyuo Vikuu. Aidha, alisema mwaka 2004, Umoja wa Afrika ulipitisha Kiswahili kiwe ni lugha ambayo itatumika katika mikutano na shughuli mbalimbali. “Je, serikali imejiandaa vipi kupeleka wakalimani wa kutosha kutoka Tanzania ili waweze kujipatia ajira?” alihoji. Akijibu maswali hayo, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makala alisema jitihada zinafanywa na taasisi hizo za kukuza Kiswahili mojawapo kuandika vitabu vingi vya kufundishia na kuongeza wataalamu. “Nasema wazo hilo tumelipokea...
TUPE MAONI YAKO

MOTO MKALI WATIKISA MAENEO YA KARIAKOO JIJINI DAR

Hali ikiwa tete. Moto ukiunguza paa la baa hiyo. Shock  ya umeme ikitokea karibu na jengo hilo. Watu waliojaa kushuhudia tukio hilo. Moto mkubwa umezuka jijini Dar es Salaam karibu kabisa na Soko Kuu la Kariakoo leo asubuhi na kuteketeza baa moja. Chanzo cha moto huo inadaiwa kuwa ni hitilafu ya umeme iliyotokea jirani na baa hiy...
TUPE MAONI YAKO

No comments:

Post a Comment