EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Monday, February 24, 2014

HAYA NI MANENO MAKALI SANA YA DR:SLAA KWA SERIKALI


Iringa. Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa amesema tatizo la umaskini linalowakabili Watanzania, linatokana na viongozi walioko madaraka kutokuwa waadilifu.
Alisema Tanzania ni nchi iliyojaaliwa rasilimali nyingi ambazo kama zikisimamiwa vyema taifa haliwezi kuwa na watu maskini kama ilivyo hivi sasa.
Dk Slaa alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza kwenye mikutano ya kampeni iliyofanyika katika Vijiji vya Igula katika Kata ya Luwota na Magulilwa mkoani Iringa.
“Nchi hii siyo maskini, imejaliwa rasilimali nyingi ambazo kama zikisimamiwa ipaswavyo, taifa lisingekuwa na umaskini kama ilivyo sasa,” alisema Dk Slaa na kuongeza:
“Leo hii viongozi wa CCM wamekosa uadilifu ndiyo maana magogo kutoka katika misitu yetu yanaibiwa na kupelekwa nje ya nchi.
Dk Slaa alisema hayo yanatokana taifa kuongozwa na watu wasio waadilifu, huku Amiri Jeshi Mkuu ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano, Jakaya Kikwete akishindwa kukabiliana na hali hiyo. Katika mikutano hiyo, Dk Slaa aliwataka wakazi wa Kalenga kumchagua mbunge wao ili kuongeza idadi ya wabunge wake
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amewataka wananchi wa Jimbo la Kalenga mkoani hapa kutambua kuwa chama hicho kipo kwa lengo la kuwatetea wananchi bila kujali itikadi za vyama.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Ifunda, Dk. Slaa alilitaka jeshi la Polisi kutenda haki kwa vyama vyote kutokana na kauli ya Rais Jakaya Kikwete kuwataka wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wajibu mapigo ya wapinzani pale wanaposhambuliwa.
Alisema Jeshi la Polisi lisitumie kauli hiyo kuwanyanyasa wapinzani.
Aliwata wananchi wa Ifunda kutambua mbunge wanayemuhitaji awe na vigezo vya kujenga hoja za kuwatetea na kuwaletea maendeleo.
Wakati huo huo, Chifu wa kabila la Wahehe, Abdu Sapi Mkwawa, amevitaka vyama vilivyosimamisha wagombea Kalenga kuendesha kampeni zao kwa amani na utulivu, na akatoa baraka zake kwa mgombea wa CHADEMA na kumtakia ushindi katika Jimbo la Kalenga.

No comments:

Post a Comment