EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Thursday, February 27, 2014

CHELSEA YATANGAZA UBABE ENGLAND UEFA CHAMPIONZ LIGI


BAADA Klabu zote za England, Arsenal, Manchester City na Manchester United, zote kupigwa Bao 2-0 kwenye Mechi za Kwanza za UEFA CHAMPIONZ LIGI, Raundi ya Mtoano Timu 16, Usiku huu Chelsea ‘waling’ara’ baada kutoka Sare 1-1 huko Türk Telekom Arena Ali Sami Yen Spor Kompleksi, Jijini Istanbul, Uturuki, walipocheza na Galatasaray Spor Kulübü.
Huko Türk Telekom Arena Ali Sami Yen Spor Kompleksi, Jijini Istanbul, Uturuki, Chelsea walitangulia kufunga kwa Bao la Dakika ya 9 la Fernando Torres kufuatia ushirikiano mzuri wa Andre Schurrle aliempasia Fulbeki aliepanda juu, Cezar Azpilicueta, ambae huku Kipa Fernando Muslera akiwa ametoka Golini, alimpasia, Fernando Torres aliemalizia vizuri.

Bao hilo, ambalo lilidumu hadi Haftaimu, pia lilichangiwa na makosa ya Beki wa zamani wa Arsenal, Emmanuel Eboue.

Katika Dakika ya 54, Galatasaray walisawazisha baada ya Kona ya Wesley Sneijder kukoswa na Jerry Terry na Aurelien Chedjou kuunganisha wavuni.

Mchezaji wa zamani wa Chelsea, Didier Drogba, ambae hakuwika, alibadilishwa katika Dakika 10 za mwisho na kuingizwa Umut Bulut.

VIKOSI:

Galatasaray: Muslera, Alex, Balta, Chedjou, Eboue, Sneijder, Inan, Felipe Melo, Hajrovic, Drogba, Burak Yilmaz

Akiba: Ceylan, Gulselam, Bulut, Kaya, Kurtulus, Colak, Sarioglu.

Chelsea: Cech, Azpilicueta, Cahill, Terry, Ivanovic, Hazard, Lampard, Ramires, Willian, Schurrle, Torres

Akiba: Schwarzer, Cole, Oscar, Mikel, Ba, Eto'o, Kalas.

Refa: Carlos Velasco Carballo (Spain)

UEFA CHAMPIONZ LIGI

Raundi ya Mtoano ya Timu 16

MARUDIANO

[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]

[Saa za Bongo]

Jumanne Machi 11

22:45 Bayern Munich v Arsenal FC [2-0]

22:45 Atletico de Madrid v AC Milan [1-0]

Jumatano Machi 12

22:45 FC Barcelona v Manchester City [2-0]

22:45 Paris Saint-Germain v Bayer 04 Leverkusen [4-0]

Jumanne Machi 18

22:45 Chelsea FC v Galatasaray Spor Kulübü [1-1]

22:45 Real Madrid CF v Schalke 04 [1-6]

Jumatano Machi 19

22:45 BV Borussia Dortmund v Zenit St. Petersburg [4-2]

22:45 Manchester United v Olympiacos CFP [0-2]


No comments:

Post a Comment