WAZIRI MKUU MSTAHAFU: EDWARD LOWASA |
MWENYEKITI wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Edward Lowassa,
amesema anakerwa na tabia ya serikali kufungia magazeti na amemfunda Naibu
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Juma Nkamia na kumtaka amalize
vifungo visivyo na mwisho vya baadhi ya vyombo vya habari nchini.
Pia
waziri mkuu huyo wa zamani, amemtaka Nkamia ahakikishe katika majukumu yake
mapya ya unaibu waziri anamshauri vizuri waziri wake kuhakikisha wanamaliza
migogoro iliyopo baina ya wizara na vyombo vya habari nchini.
Lowassa
alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam wakati kamati yake ikimuaga Juma
Nkamia aliyekuwa mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo kabla ya hivi karibuni Rais
Jakaya Kikwete kumteua kuwa naibu waziri wa wizara hiyo.
Lowassa
alisema si jambo jema kwa vyombo vya habari kuendelea kukaa katika vifungo
visivyojulikana mwisho wake katika zama hizi ambapo uhuru wa vyombo vya habari
unatakiwa upewe kipaumbele.
Aliongeza
kuwa ni wakati muafaka kwa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
wakaanzisha majadiliano ya kutafuta muafaka na makundi yote yanayojihusisha na
masuala ya habari.
Kwa
upande wake, Waziri Nkamia alisema licha ya kuwa na siku sita ofisini tangu
aanze kazi katika wizara hiyo, ameshaomba mrejesho wa sheria iliyotumika
kuyafungia baadhi ya magazeti kwa ajili ya mapitio zaidi.
Pia
ameahihidi kumshauri Waziri wake, Fenella Mukangara, akutane na wahariri wa
vyombo vya habari kwa ajili ya kumaliza tofauti zao.
Alisema
ni aibu kwa kiongozi wa serikali kuacha kuandikwa au kutangazwa na baadhi ya
vyombo vya habari kwa sababu ya tofauti ya kimtazamo.
Ushauri
wa Lowassa kwa Naibu Waziri Nkamia umekuja ikiwa ni takriban mwaka mmoja na
nusu umepita tangu serikali ilipolifungia gazeti la Mwanahalisi kwa muda
usiojulikana, kwa madai ya kuandika habari zilizotafsiriwa kuwa ni za
uchochezi, uhasama na uzushi dhidi ya serikali.
Katika
kulifungia Mwanahalisi, serikali ilitumia Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976,
kifungu Na. (25) (i).
Kifungu
hicho ndicho kinacholalamikiwa na wadau wa habari kuwa kinanyima uhuru wa
vyombo vya habari na kwamba ndiyo sheria iliyokuwa ikitumiwa na wakoloni
kuwazuia viongozi wa TANU kutoa maoni.
Kwa
mfano, mwaka 1958 Tanganyika ikiwa chini ya ukoloni wa Waingereza, Mwalimu
Julius Nyerere alishtakiwa kwa kukashifu baada ya kuandika makala iliyodaiwa
kuwakashifu wakuu wa wawili wa wilaya.
Mwalimu
Nyerere wakati huo alikuwa mhariri wa gazeti la Sauti ya TANU na alishtakiwa
kwa vifungu vya uchochezi vilivyoingizwa pia kwenye Kanuni ya adhabu ya sasa na
Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976.
Kwa
kosa hilo, Mwalimu Nyerere alihukumiwa kifungo cha miezi sita jela au kulipa
faini ya paundi 150. Nyerere alimaliza kesi hiyo kwa kulipa faini.
Baada
ya uhuru, si Mwalimu Nyerere wala marais waliofuatia waliokubali kubadilisha
sheria hizo, bali zimeendelea kuwatafuna Watanzania kila mara.
>>Tanzania daima
>>Tanzania daima
No comments:
Post a Comment