EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Sunday, November 10, 2013

WATU 10,000 WAFARIKI DUNIA KWA KIMBUNGA

Watu zaidi ya 10,000 wameripotiwa kufariki dunia nchini Ufilipino katika jimbo la Leyte, baada ya dhoruba ya kimbunga kikali cha Haiyan kuikumba nchi hiyo, na kusababisha pia uharibifu mkubwa. 


Mkoa wa kati wa Leyte ni miongoni mwa maeneo yaliyoathiriwa zaidi na kimbunga hicho, kilichoanzia mashariki na kuelekea hadi magharibi mwa Ufilipino.
Barabara za mji wa Tacloban mkoani humo zimefunikwa na maji au hazipitiki, kutokana na kuangukiwa na miti huku maiti za watu zikiwa zimetapakaa huku na kule. 

Watu wapatao laki nane walilazimishwa kuyahama makazi yao katika tahadhari iliyochukuliwa kukabiliana na kimbunga cha Haiyan.
Sebastian Rhodes Stampa, mkuu wa timu ya Umoja wa Mataifa ya Uratibu wa Tathmini ya Maafa aliyeko Tacloban amesema ukubwa wa maafa kama hayo yaliyosababishwa na kimbunga cha Haiyan aliyashuhudia baada ya Tsunami iliyotokea katika Bahari ya Hindi. 

No comments:

Post a Comment