EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Wednesday, January 29, 2014

Nchimbi akabidhi ofisi rasmi kwa Mhe. Mathias Chikawe



Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Dkt. Emmanuel Nchimbi akitoa neno fupi wakati wa hafla fupi ya Makabidhiano rasmi ya Ofisi kwa Waziri Mpya wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Mhe. Mathias Chikawe(wa pili kulia). Hafla hiyo imefanyika leo Januari 27, 2014 katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, Jijini Dar es Salaam.
Waziri Mpya wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe akitoa maelezo mafupi mbele ya Waandishi wa Habari kabla ya kumkaribisha aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Dkt. Emmanuel Nchimbi katika hafla fupi ya Makabidhiano ya Ofisi leo Januari 27, 2014 Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na Idara zilizo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakimsikiliza aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Dkt. Emmanuel Nchimbi wakati wa hafla ya Makabidhiano rasmi ya Ofisi leo Januari 27, 2014 Jijini Dar es Salaam(wa kwanza kulia) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja.
Baadhi ya Watumishi Waandamizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakimsikiliza aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Dkt. Emmanuel Nchimbi(hayupo pichani) katika hafla fupi ya Makabidhiano rasmi ya Ofisi leo Januari 27, 2014 Jijini Dar es Salaam( Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

No comments:

Post a Comment