Aliyekuwa
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Dkt. Emmanuel Nchimbi akitoa neno fupi
wakati wa hafla fupi ya Makabidhiano rasmi ya Ofisi kwa Waziri Mpya wa Wizara
ya Mambo ya Ndani, Mhe. Mathias Chikawe(wa pili kulia). Hafla hiyo imefanyika
leo Januari 27, 2014 katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, Jijini
Dar es Salaam.
Waziri
Mpya wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe akitoa maelezo
mafupi mbele ya Waandishi wa Habari kabla ya kumkaribisha aliyekuwa Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Dkt. Emmanuel Nchimbi katika hafla fupi ya
Makabidhiano ya Ofisi leo Januari 27, 2014 Jijini Dar es Salaam.
Baadhi
ya Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na Idara zilizo chini ya Wizara
ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakimsikiliza aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya
Nchi, Mhe. Dkt. Emmanuel Nchimbi wakati wa hafla ya Makabidhiano rasmi ya Ofisi
leo Januari 27, 2014 Jijini Dar es Salaam(wa kwanza kulia) ni Kamishna Jenerali
wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja.
Baadhi
ya Watumishi Waandamizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakimsikiliza
aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Dkt. Emmanuel Nchimbi(hayupo
pichani) katika hafla fupi ya Makabidhiano rasmi ya Ofisi leo Januari 27, 2014
Jijini Dar es Salaam( Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).
No comments:
Post a Comment