ASERNAL WENGER |
KLABU ya Arsenal inajiamini beki wake tegemeo, Per Mertesacker atasaini Mkataba mpya wa muda mrefu.
Klabu
hiyo imeanza mazungumzo na mwanasoka huyo wa kimataifa wa Ujerumani juu
ya vipengele vya Mkataba na inafahamika mazungumzo yanaendelea vizuri.
Mertesacker
amedhihirisha yeye ni mwamba wa safu ya ulinzi ya The Gunners
akitengeneza ukuta mgumu wa mabeki wanne akicheza sambamba na Laurent
Koscielny.
Na
ikiwa mambo yote yatakwenda kama ilivyopangwa, Mertesacker atasaini
Mkataba mpya wa miaka minne, ambao utahusisha kupanda kwa maslahi yake
kabla ya mwisho wa mwaka huu.
Baada
ya kuwa mwanzo na mgumu Uwanja wa Emirates, hatimaye beki huyo wa nguvu
wa kati amefanikiwa kuteka hisia za mashabiki wa klabu hiyo ya London
Kaskazini- akifanya kazi nzuri mwanzoni mwa msimu huu.
Mkali kweli: Baada ya mwanzo mgumu Arsenal, beki huyo Mjerumani sasa mambo yanamuendea vizuri Emirates
No comments:
Post a Comment