MKURUGENZI mkuu wa klabu
ya Juventus, Giuseppe Marotta anaamini kuwa mshambuliaji nyota wa timu
hiyo Paul Pogba ana nafasi ya kushinda taji la Ballon d’Or siku za
mbele.
Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye miaka 20 alishinda
tuzo Golden Boy mapema wiki hii mbele ya wachezaji wengine waliokuwa
wakigombea tuzo hiyo kama Romelu Lukaku na Julian Draxler.
Marotta
amesema hana shaka kuwa Pogba ataweza kunyakuwa tuzo hiyo kubwa kabisa
kwa wachezaji katika siku za mbele na ni mategemeo yake atafikia
mafanikio hayo wakiwa naye hapo Juventus.
Pogba alijiunga na Juventus
akitokea Manchester United katika kipindi cha majira ya kiangazi mwaka
2012 na toka kipindi hicho ameshacheza mechi 50 kwa mabingwa hao wa
Serie A.
No comments:
Post a Comment