KIUNGO mahiri wa klabu
ya Bayern Munich, Arjen Robben anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa muda
baada ya kuumia goti katika mchezo wa jana.
Robben mwenye umri wa miaka
29 aliifungia Bayern bao katika dakika ya nne kwenye mchezo wa Kombe la
Ujerumani dhidi ya Augsburg lakini alitolewa kwa machela dakika 12
baadae kwa kugongana na golikipa wa timu pinzani Marwin Hitz.
Madaktari
wa timu hiyo wamedai kuwa baada ya kufanyiwa vipimo zaidi ndipo
wanatajua ni muda gani nyota huyo atakaa nje ya uwanja. Robben amekuwa
katika kiango cha juu katika mechi za hivi karibuni akiwa amefunga bao
katika mechi zilizopita.
No comments:
Post a Comment