EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Wednesday, December 11, 2013

ONGEZEKO LA KURIPOTI VITENDO VYA UKATILI NA UNYANYASAJI WA KIJINSIA LAFIKIA 14.7% MKOANI ARUSHA.




 Na shafii mohamed    ,Arusha
Jumla ya kesi 507 zinazohusiana na matukio ya ukatili na unyanyasaji wa Kijinsia zimeripotiwa katika Dawati la Jinsia na Watoto la Mkoa wa Arusha ambapoTakwimu hizo ni toka Novemba 2012 hadi Novemba 2013 mwaka huu.
mkaguzi wa jeshi la polisi Dawati la jinsi na watoto  Bi Honorina Msoka  akitoa zawadi kwa baadhi ya wagonjwa  walio lazwa wold ya kina mama na watoto  katika  Hospitali ya mkoa wa Arusha mountimeru
Hayo yalielezwa na Mkuu wa kitengo hicho Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Mary Lugola wakati watendaji wa ofisi hiyo walipoungana na wadau mbalimbali duniani kuadhimisha siku 16 za kupinga Ukatili na Unyanyasaji wa Kijinsia walipotembelea Shirika lisilo la Kiserikali la Faraja centre linaloshughulika na malezi ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu na wasichana waliojifungua wakiwa na umri mdogo pamoja na wagonjwa waliolazwa katika hospitali ya Mkoa ya Mount Meru.

Akitoa ufafanuzi kuhusiana na kesi hizo alisema kwamba, idadi hiyo imeongezeka kwa asilimia 14.7 ikilinganishwa na Novemba 2011 hadi Novemba 2012 ambapo kesi 442 ziliripotiwa.

 Alisema ongezeko hilo linatokana na elimu inayotolewa mara kwa mara na Ofisi hiyo kwa wananchi kupitia mikutano na vyombo vya habari hali iliyowafanya wananchi wahamasike kupinga vitendo vya ukatili na unyanyasaji kwa kutoa taarifa katika Ofisi hiyo. 
mkuu wa kitengo na mwenyekiti wa askari wanawake  na mrakibu mwandamizi wa jeshi la polisi  mkoa wa Arusha  (ssp) mary Lugola  akikabidhi zawad msimamizi na mkuu wakituo cha FARAJA WOMEN GROUP Bi Martina Siara

Alisema kati ya kesi hizo, kesi zilizokuwa zinawahusu wanawake ni 280 wakati wanaumeni 120 huku watoto ni 107. Miongoni mwa kesi hizo tayari kesi 132 zimekwishafikishwa mahakamani huku kesi 375 zinaendelea kupelelezwa.

Mkuu huyo wa Dawati la Jinsia na Watoto (SSP) Mary Lugola alisema kwamba miongoni mwa kesi zinazoripotiwa katika ofisi hiyo ni pamoja na ubakaji, kulawiti, ukatili dhidi ya mtoto, migogoro katika ndoa na kadhalika.

Akizungumza wakati anawatembelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu na wasichana waliojifungua wakiwa na umri mdogo ambao wanalelewa na Shirikalisilo la Kiserikali la Faraja na wagonjwa waliolazwa katika Wodi ya Watoto hospitali ya Mkoa ya Mount Meru, (SSP) Mary Lugola alisema kwamba katika kuonyesha kujali kitengo cha Dawati kimeamua kuungana nao kwa kuwatembelea na kutoa zawadi mbalimbali kwa makundi hayo.

Kwa upande wake msimamizi wa Shirika lisilo la Kiserikali la Faraja Young Women Development Organization Bi. Martina Siara alilishukuru jeshi la Polisi mkoani hapa kitengo cha Dawati kwa jinsi linalovyoshirikiana na kituo hicho cha Faraja katika katika suala zima la ulinzi pamoja na utoaji wa elimu na ushauri kwa wanafunzi waliopo kituoni hapo hivyo kuwapa mwanga kuhusiana na haki zao.

Jeshi la Polisi kupitia kitengo cha Dawati Mkoani hapa limeadhimisha siku 16 za kupinga Ukatili na Unyanyasaji wa Kijinsia kwa kutembelea kituo cha Faraja na wodi ya watoto katika hospitali ya Mount Meru kwa kutoa zawadi mbalimbali kwa watoto wa kituo hicho pamoja na wagonjwa waliolazwa hospitalini hapo huku likiwa na kauli mbiu ya jeshi hilo nchini isemayo “Zinduka tumia Dawati la Jinsia na Watoto kukemea Ukatili wa Jinsia na Watoto.

No comments:

Post a Comment