EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Monday, November 25, 2013

SUDANI YAJIPANGA KUPAMBANA NA WAASI NCHINI HUMO



Gavana wa jimbo la Kordofan Kusini nchini Sudan, amesisitiza juu ya kupambana na makundi ya waasi jimboni humo, na kusisitiza kuwa hatawavumilia waasi vyovyote iwavyo. 


Adam Al-Faki ameongeza kuwa, idara ya kieneo ya jimbo hilo imepanga mikakati madhubuti kwa ajili ya kulisafisha jimbo hilo kutokana na uwepo wa makundi ya wabeba silaha.Ameitaja mikakati hiyo kuwa ni pamoja na kuwaachilia huru watuhumiwa wa ujasusi, kuwarejesha kazini baadhi ya watu waliokuwa wamefutwa kazi, kuimarisha usalama na uthabiti na kuinua kiwango cha kujiamini jimbo hilo.Hata hivyo amesema kuwa, makundi ya wabeba silaha yamekuwa yakikwamisha mikakati hiyo ikiwemo kutekeleza mashambulizi dhidi ya  baadhi ya miji na mauaji ya watu wasio na hatua.

No comments:

Post a Comment