EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Monday, November 25, 2013

MUBARACK NA WANAWE WAWILI KUFIKISHWA KIZIMBANI TENA



Majaji nchini Misri wamesema kiongozi wa zamani wa nchi hiyo Hosni Mubarak pamoja na wanawe wawili, atapandishwa tena kizimbani, kwa tuhuma za kuhodhi na kupora mali za taifa hilo. 
 
Rais wa zaman wa Misri-Hosni Mubarack
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Mubarak na wanawe ambao ni Alaa na Gamal wanatuhumiwa kupora kiasi cha Lira milioni 125 za nchi hiyo, sawa na Euro milioni 13, kutoka katika ofisi ya rais.
Uchunguzi unaonesha kuwa, watuhumiwa wanne wengine wa faili hilo, ni watu waliomsaidia Mubarak na wanawe katika uporaji wa kiasi hicho cha fedha.Ikumbukwe kuwa, Mubarak pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani wa serikali yake na watu wengine sita katika uongozi uliopita, wanatuhumiwa kushiriki katika mauaji dhidi ya waandamanaji katika machafuko ya mwaka 2011, yaliyopelekea kung’olewa madarakani kwa utawala wake.

No comments:

Post a Comment