EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Monday, November 25, 2013

RAIS BOUBACAR KEITA AFURAHISHWA NA WANANCHI WAKE KATIKA UCHAGUZI



Rais wa Mali Ibrahim Boubacar Keïta ameeleza, kufurahishwa na ushiriki mkubwa wa wananchi katika uchaguzi wa bunge uliofanyika hapo jana nchini humo. 


Rais Keïta ametangaza hayo akiwa mjini Bamako na kuongeza kuwa, hivi sasa taifa la Mali limesimama kwa miguu yake.
Rais huyo amesema kuwa, uchaguzi wa bunge utasaidia kuimarisha hali ya amani nchini Mali.Jana wananchi wa Mali walipiga kura kuwachagua wawakilishi wao wa Bunge wanaowania viti 147, ambapo jumla ya wagombea elfu moja walijitokeza kuwania viti hivyo.
Karibu watu milioni sita na laki tano, walikuwa wametimiza masharti ya kupiga kura.Baadhi ya duru za habari zimeripoti kuwepo ushiriki mdogo wa wapiga kura katika baadhi ya maeneo kutokana na kuwepo vitisho vya kutokea miripuko ya kigaidi.

No comments:

Post a Comment