EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Tuesday, October 22, 2013

WAASI NCHINI MSUMBIJI WASEMA MAKUBALIANO YA AMANI YAMEVUNJIKA



Waasi wa zamani wa renamo nchini msumbiji wamesema kuwa, makubaliano ya amani yaliyowekwa mwaka 1992 kati ya kundi hilo na serikali ya msumbiji yamevunjika, baada ya majeshi ya serikali kushambulia ngome za waasi hao wa zamani wa msumbiji. 
 
Raisi wa msumbiji Almando Guebuza
Msemaji wa renamo fernando mazanga amesema kuwa, viongozi wa ngazi za juu wa renamo wanafikiria pia uwezekano wa kususia uchaguzi wa serikali za mitaa uliopangwa kufanyika mwezi ujao, iwapo hayatafanyika mabadiliko ya kimsingi kwenye sheria za uchaguzi nchini humo.
Matamshi ya msemaji wa renamo yanaashiria uwezekano wa kuanza tena mapigano ya ndani nchini humo.



Wakati huohuo, jeshi la msumbiji likitumia vifaru limezingira makao ya afonso dhlakama kiongozi wa renamo yaliyoko katika eneo la satunjira.
Inafaa kuashiria hapa kuwa, waasi wa zamani wa renamo kwa muda wa miaka 16 walikuwa wakipambana na majeshi ya serikali ya msumbiji, hadi yalipofikiwa makubaliano ya amani mwaka 1992.

No comments:

Post a Comment