EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Tuesday, October 22, 2013

MGOGORO WA KISIASA WASABABISHA WATOTO MILIONI 1 NA NUSU KUTOKWENDA SHULE



Mfuko wa watoto umoja wa mataifa (unicef) umetangaza kuwa, karibu watoto milioni moja na  nusu wa madagascar wanashindwa kwenda shuleni kutokana na umasikini na mgogoro wa kisiasa ulioikumba nchi hiyo katika miaka ya hivi karibuni. 


Mwakilishi wa unicef nchini madagascar stephen lauwerier amesisitiza kuwa, katika mwaka 2008 na kabla ya kuanza mgogoro wa kisiasa nchini humo, jumla ya watoto milioni nne walikuwa wakisoma katika shule za msingi nchini humo.    Taarifa hiyo ya unicef imetolewa zikiwa zimesalia siku chache kabla ya kufanyika uchaguzi wa rais nchini humo.
Imeelezwa kuwa, uchaguzi wa rais nchini humo umepangwa kufanyika siku ya ijumaa oktoba 25 mwaka huu.  Waangalizi wa uchaguzi kutoka umoja wa afrika walioko hivi sasa nchini humo, wataendelea kubaki nchini madagascar kwa muda mrefu zaidi hata baada ya kutangazwa matokeo ya uchaguzi huo, ili kuhakikisha amani na utulivu unarejea nchini humo.
 

No comments:

Post a Comment