VITA NCHINI KONGO NA M23 YAANZA UPYA TENA KWA KASI
 |
| kikosi cha waasi wa M23 |
Mapigano kati ya waasi wa harakati ya Machi
23 na jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yameanza tena hii leo.Ripoti zinaarifu kuwa hadi jioni ya leo
mapigano yalikuwa yakiendelea huko Kibumba umbali wa kilomita 15 kutoka mji wa
Goma kati ya jeshi la Kongo na waasi wa M23. Msemaji wa jeshi la Kongo
amethibitisha kutokea mapigano hayo na kutangaza kuwa jeshi hilo limejizuia
kutekeleza mashambulizi lakini akasema kuwa waasi wa Machi 23 watakabiliwa na
mashambulizi ya jeshi la Kongo iwapo wataendeleza uchokozi.
 |
| kikosi cha waasi wa M23 |
Waasi wa harakati ya Machi 23 pia
wamelituhumu jeshi la Kongo na kusema kuwa jeshi hilo ndilo lililoanzisha mashambulizi
hayo ya leo. Ni muda sasa maeneo ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Kongo yanashuhudia harakati za wanamgambo wenye silaha hususan wale wenye
uhusiano na waasi wa M23.
No comments:
Post a Comment