Rais
joyce banda wa malawi ametishiwa kuuawa, baada ya kutekeleza mikakati yake ya
kufichua na kupambana na ufisadi uliokithiri nchini humo.
Waziri
wa habari wa malawi brown mpinganjira, amethibitisha habari hizo na kusema kuwa,
mafisadi wameanza kutishia maisha ya kiongozi huyo wa malawi, kutokana na
msimamo wake wa kuvunja baraza la mawaziri na kufichua ufisadi mkubwa wa
kifedha uliofanywa na viongozi waandamizi nchini humo.
Mpinganjira
amesema kuwa, baadhi ya vitisho hivyo vimetolewa toka nje ya nchi hiyo na jeshi
la polisi linaendelea na uchunguzi na hatimaye kubaini wahusika wa njama hizo.
Inafaa
kuashiria hapa kuwa, tarehe 10 oktoba mwaka huu, rais joyce banda aliamua
kulivunja baraza la mawaziri baada ya kufichuliwa kwa kashfa ya ufisadi wa dola
milioni tatu, uliofanywa na viongozi wa ngazi za juu wa serikali ya malawi. Joyce
banda anayehesabiwa kuwa rais wa kwanza mwanamke nchini humo, aliingia
madarakani mwaka 2012 baada ya kufariki dunia bingu wa mutharika rais wa zamani
nchini humo.

No comments:
Post a Comment