EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Tuesday, August 12, 2014

MEMBE ,NAPE WAHANI MISIBA KWA WALIOPGONGWA NA GARI MTAMA.

:Mbunge wa Jimbo la Mtama mkoani Lindi ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.Mhesimiwa Bernard Membe akimjulia hali na kumpa pole Ndugu Shaaban Issa mmoja wa majeruhi watatu wa ajali ya a gari iliyotokea Mtama na kusababisha vifo vya watu 8.
Mbunge wa Jimbo la Mtama mkoani Lindi ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.Mhesimiwa Bernard Membe pamoja na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa Nape Nnauye wakizungumza na waginjwa waliolazwa  kwenye hospitali ya Nyangao mkoani Lindi ambapo wengi wao ni wa ajali za pikipiki.
Mbunge wa Jimbo la Mtama mkoani Lindi ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.Mhesimiwa Bernard Membe pamoja na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa Nape Nnauye wakimsikiliza Mzee Selemani Chitanda ambaye ameondokewa na mtoto wake wa kiume Maliki S. Chitanda kwenye ajali mbaya ya gari lililoacha njia wakati dereva akijaribu kumkwepa mbuzi na kusababisha vifo vya watu 8.
Mbunge wa Jimbo la Mtama mkoani Lindi ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.Mhesimiwa Bernard Membe akiongozana na  Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa Nape Nnauye kwenda kutoa salaam za rambirambi kwa familia zilizopoteza jina wao kwenye agari ya gari iliyotokea Mtama,kulia ni  Mwenyekiti wa Bodi ya Washauri wa Madini,Richard Kasesela .
Watu 8 wamepoteza maisha na wengine watatu kujeruhiwa kwenye ajali ya gari iliyotokea Mtama tarehe 8/8/2014
g5.Mbunge wa Jimbo la Mtama mkoani Lindi ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.Mhesimiwa Bernard Membe akisalimiana na Salum Said Mchora ambaye amepoteza mtoto wake wa kiume mwenye umri wa miaka 23 Said S. Mchora  mkazi wa Masasi,Majengo.
 Watu 8 wamepoteza maisha na wengine watatu kujeruhiwa kwenye ajali ya gari iliyotokea Mtama tarehe 8/8/2014
Picha na Adam H. Mzee

VODACOM YAMKABIDHI WAZIRI CHIKAWE MAMILIONI YA WIKI YA NENDA KWA USALAMA BARABARANI





Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (wapili kulia) akimshukuru Ofisa wa Mawasiliano na Uhusiano wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Georgia Mutagahywa (kushoto) baada ya kupokea hundi yenye thamani ya Sh. Milioni 40 msaada uliotolewa kwa ajili ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani inayotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Septemba mwaka huu, jijini Arusha. Wapili kushoto ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu, na kulia ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Naibu Kamishna, Mohamed Mpinga. Makabidhiano hayo yalifanyika katika Ukumbi wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (wapili kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) baada ya kupokea hundi ya Sh. Milioni  kwa ajili ya maandalizi ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani, kutoka kwa Ofisa wa Mawasiliano na Uhusiano wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Georgia Mutagahywa (watatu kulia). Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani  inatarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Septemba mwaka huu, jijini Arusha. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil. Wapili kushoto ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu, na kushoto ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Naibu Kamishna, Mohamed Mpinga. Makabidhiano hayo yalifanyika katika Ukumbi wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Picha zote na Felix Mwagara wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

PICHA ZOTE NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

LIVERPOOL YAMTAKA ETO'O.

KLABU ya Liverpool inafanya majadiliano ya kutaka kumchukua Samuel Eto’o katika kipindi hiki ambacho wanahitaji kusajili mshambuliaji. Eto’o kwasasa yuko huru baada ya kuachwa na Chelsea mwishoni mwa msimu uliopita na anaweza kuongeza uzoefu katika kikosi cha Liverpool kinachonolewa na Brandan Rodgers. Rodgers amekuwa akitafuta mshambuliaji toka dili na Loic Remy lilipokwama na Eto’o anaweza kuchagua lao sahihi. Uzoefu wa nyota huyo mwenye umri wa miaka 33 hususani mataji matatu aliyoshinda ya Ligi ya Mabingwa Ulaya unaweza kumsaidia kwasababu Liverpool imerejea katika michuano hiyo baada ya miaka mitano na hawana wachezaji wa kutosha wenye uzoefu nayo. Mbali na Liverpool kuonyesha nia na Eto’o, Inter Milan na Ajax Amsterdam nazo pia zimezungumza na wawakilishi wa mchezaji huyo.
CABALLERO ATAMBA KUCHUKUA NAMBA YA JOE HART, CITY.
GOLIKIPA mpya Willy Caballero ana hamu kubwa ya kuchukua nafasi ya Joe Hart kama golikipa namba moja wa Manchester City msimu huu. Kipa huyo wa kimataifa wa Argentina alisajiliwa akitokea Malaga Julai ambapo alicheza katika mechi yake ya kwanza ya kimashindano akiwa na mabingwa hao wa Ligi Kuu wakati walipotandikwa mabao 3-0 na Arsenal katika mchezo wa Ngao ya Jamii. Caballero amesema anatamani kuendelea kubakia katika nafasi hiyo wakati kikosi cha City kinachonolewa na Manuel Pellegrini kitakapoanza kutetea taji lake katika mchezo dhidi ya Newcastle United Agosti 17 mwaka huu. Kipa huyo alikiri kuwa anataka kuwa namba moja wakati akihojiwa na atafanya mazoezi kwa bidii ili kuhakikisha anamshawishi kocha wake kumpa nafasi ya kuanza.
CHAMA CHA SOKA ITALIA CHAPATA RAIS MPYA.
CHAMA cha Soka nchini Italia kimepata rais mpya Carlo Tavecchio aliyetangazwa jana. Tavecchio mwenye umri wa miaka 71 alikuwa makamu wa rais wa shirikisho hilo toka mwaka 2009 lakini alithibitisha kugombea kugombea nafasi hiyo kufuatia uamuzi wa Giancarlo Abete kuamua kujiuzulu baada ya Italia kutolewa mapema katika michuano ya Kombe la Dunia iliyofanyika Brazil Juni mwaka huu. Pamoja na kampeni zilizojaa utata huku akituhumiwa kwa masuala mbalimbali Tavecchio alipambana na kuhakikisha anamshinda mpinzani wake ambaye ni nyota wa zamani wa AC Milan Demetrio Albetini na kuteuliwa kuwa rais mpya wa FIGC. Kibarua cha kwanza cha Tavecchio kitakuwa ni kusaidia kutafutwa kwa kocha mpya wa timu ya taifa ya nchi hiyo huku kocha wa zamani wa Juventus Antonio Conte akipewa nafasi kubwa ya kuchukua nafasi hiyo.
GFA YAUNDA KAMATI KUIIMARISHA BLACK STARS.
CHAMA cha Soka nchini Ghana-GFA kimeunda kamati ya watu watatu itakayokuwa na jukumu la kuteua mshauri wa ufundi katika kikosi cha timu ya taifa ya nchi hiyo, Black Stars. Hata hivyo maofisa wa GFA wamesisitiza kuwa mshauri wa ufundi atakayeteuliwa atakuwa na jukumu la kusimamia mfumo mzima wa Stars na sio kocha pekee. Umuazi wa kuteua kamati hiyo kwa mujibu wa taarifa ya GFA umepelekwa katika kikao cha kamati ya utendaji ya chama hicho kufuatia kupitia muelekeo wa ufundi wa kikosi cha timu ya taifa. Kamati hiyo ya watu watatu itaongozwa na makamu wa rais wa GFA Fred Crentsil ambaye atafanya kazi sambamba na Fred Pappoe na Francis Oti Akenteng. Taarifa ya GFA iliendelea kudai kuwa kamati hiyo itafanya pamoja na kocha wa Black Stars Kwesi Appiah ili kutafuta mtu atakayeweza kuipeleka timu ya taifa katika muelekeo unaofaa.
ANCELOTTI AWASHUSHUA WANAOMTAKA KHEDIRA, ADAI HANA MPANGO WA KUMUUZA.
MENEJA wa klabu ya Real Madrid, Carlo Ancelotti amevionya vilabu vya Arsenal na Chelsea kumuacha Sami Khedira kwani kiungo huyo hauzwi. Nyota huyo wa kimataifa wa Ujerumani amekuwa akihusishwa kuondoka Santiago Bernabeu toka waliposhinda Kombe la Dunia mwezi jana huku Uingereza pakitajwa kama kama uelekeo wake. Usajili wa Mjerumani mwenzake Toni Kroos kutoka Bayern Munich ndio ulionekana kuchangia kwa kiasi kikubwa nyota huyo kuhusishwa na kuondoka lakini Ancelotti amekanusha tetesi hizo na kudai kuwa Khedira bado ana mkataba nao unaomalizika kiangazi mwakani hivyo bado atabakia klabu hapo kwa kipindi hiki. Madrid wanahatarisha kumkosa Khedira bila kupata chochote kama wakishindwa kumshawishi asaini mkataba mpya wa mabingwa hao wa Ulaya wakati wa msimu 2014-2015.