EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Wednesday, August 20, 2014

KATIKA kukamilisha maandalizi ya Ligi Kuu Tanzania Bara, wageni wapya Ligi, Ndanda Fc jana wamewapima afya za wachezaji wao wote walioingia mikataba nao ya kukitumikia kikosi hicho msimu ujao wa Ligi.

NA MSHAMU NGOJWIKE
Hafla hiyo ya kupima afya jana asubuhi,ilifanyika kwenye Hospitali ya Wilaya ya Kinondoni ya ‘Mwanyamala’ ikiongozwa na viongozi wa Klabu pamoja na benchi la ufundi.
Akizungumza na SWACOTZ FORUM jana, Katibu Msaidizi wa Ndanda Fc, Selemani Kachele alisema wamefikia hatua hiyo ya kuwatambua hali zao za kiafya wachezaji wote kabla ya kuanza msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara(VPL).
“Tunapima afya zetu kwa ujumla ili kubaini matatizo ya kiafya wachezaji tuliowasajili kabla ya kuanza kwa Ligi msimu huu, uwezi kuingia kwenye vita bila kukagua silaha zako kama zina mtatizo au laa!, tunataka kutambua ufitness wao,isije mchezaji michezo miwili mitatu yupo benchi kwa maumivu,”alisema.
Aliesma taratibu hii ya kupima afya ya wachezaji itakuwa endelevu ya kubaini matatizo yao ya Kimwili kabla ya kushiriki mashindano ya aina yeyote hapa nchini.
Ndanda Fc,ipo kwenye maandalizi ya  msimu wa Ligi kuu Tanzania Bara inayotarajia kuanza kunguruma Septemba 20 mwaka huu, kwa kuweka  kambi ya siku 40, katika  Chuo Kikuu cha Ardhi jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment