MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa
Ufaransa, Karim Benzema ameongeza mkataba wa kuendelea kuichezea Real Madrid ya
huko nchini Hispania mkataba ambao utambakisha klabuni hapo hadi mwaka 2019.
Benzema amesaini mkataba huo mara baada ya kukataa kuhamia kunako timu za Ligi
Kuu nchini uingereza ambako alihusishwa na taarifa za kuhitajika na vilabu
mbalimbali vya nchi hiyo.
Hivi karibuni Kulikuwa kuna tetesi
kwamba mpachika mabao huyo wa Ufaransa anaweza kuondoka klabu hiyo ya Hispania,
lakini sasa wazi ataishi Bernabeu hadim mwaka 2019.
Hivyo kuviacha midomo wazi vilabu
vya Arsenal, Liverpool na Tottenham Hotspur vyote kutokea uingereza ambavyo ni
miongoni mwa timu za Ligi Kuu nchini humo zilizokuwa zinamtaka mchezaji huyo
mwenye umri wa miaka 26.
No comments:
Post a Comment