Mvutano mkali watokea baina ya Serikali na Bunge
Msuguano huo umeshika kasi wiki hii baada ya
Serikali kuwarudisha kwenye nyadhifa zao vigogo wawili wa Wizara ya
Maliasili na Utalii ambao hivi karibuni waliondolewa na Waziri Lazaro
Nyalandu, huku wabunge wakiapa kuibana Serikali kuwang’oa viongozi hao.
Vigogo hao ni pamoja na Mkurugenzi wa Wanyamapori,
Profesa Alexander Songorwa na Mkurugenzi Msaidizi, Jaffar Kidegesho kwa
madai ya kutowajibika ipasavyo katika vita dhidi ya ujangili nchini.
Mbali na sababu hiyo, lakini Nyalandu alikaririwa
akisema alichukua uamuzi huo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mazimio
16 ya Bunge, yaliyotolewa baada ya taarifa ya Operesheni Tokomeza
Ujangili.
Ikulu yatoa tamko
Wakati mvutano huo ukiendelea, Ikulu imeitaka wizara hiyo kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za kumfukuza mtu kazi.
Katibu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema
kuzingatiwa sheria, kanuni na taratibu za kumfukuza mtu kazi ndiyo
suluhisho la msuguano unaoendelea kati ya Waziri Nyalandu na Katibu Mkuu
wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Maimuna Tarishi juu ya hatima ya
wakurugenzi hao ambao walitimuliwa kazi Februari mwaka huu.
Balozi Ombeni aliwataka viongozi hao kuhakikisha
kuwa uamuzi wowote wanaoufanya kuhusu kuwaondoa kazini watumishi hao
unazingatia sheria, taratibu na kanuni kwa kuwa zinaeleza wazi hatua
zinazopaswa kuchukuliwa.
“Siwezi kujua kwa nini wanaendelea kuvutana, hilo
waulize wao, ninachojua wanatakiwa wazingatie sheria, kanuni na taratibu
katika jambo hilo,” alisema.
Alipoulizwa ni nani kati ya Nyalandu na Tarishi
hafuati sheria za utumishi wa umma, alisema: “We mwenyewe nenda kazisome
(sheria) utajua tu.”
Kwa mujibu Sheria ya Utumishi wa Umma ya mwaka
2002, Kifungu cha IV (23) (2) inayozungumzia mamlaka ya Rais kumwondoa
mtumishi aliyemteua kazini, amri ya kumfukuza mtumishi wa umma
itatekelezwa iwapo
(a)hati ya mashtaka imeandikwa dhidi yakeSOURCE>>>MWANANCHI
No comments:
Post a Comment