EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Sunday, May 4, 2014

MTWARA YATIKISA VIWANGO VYA ELIMU



NA: KASSIM NGUMBI
Mkuu wa wilaya ya mtwarai MH: Williman Kapenjama Ndile amezipongeza shule zilizofanya vizuri toka manispaa ya mtwara mikindani katika matokeo ya mitihani ya mwisho kwa upande wa shule za msingi na sekondari  iliyofanyika kitaifa mwishoni mwa mwaka 2013 huku akiziasa shule ambazo hazikufanya vizuri kwa mwaka huu kujipanga na kuchukulia hiyo kama sehemu ya changamoto kwao ili kufaulisha wanafunzi wao vizuri hali itakayoplekea kupanda kwa kiwango cha elimu na kufikia lengo la serikali la matokeo makubwa sasa.
Akizungumza katika sherehe za wiki ya elimu kiwilaya kwa ngazi ya wilaya zilizofanyika leo katiuka vuwanja vya mashujaa mtwara mikindani MH: Ndile ambaye pia alikuwa ninmgeni rasmi alisema kuwa mtwara ilizamiria kufanya vizuri katika elimu kwa msimu uliomalizika na inayoendelea na hicho ndicho kilivhofanyika  na kueleza kuwa ni fahari kubwa kuona shule nyingi zimeweza kufanya vizuri kuanzia zile binafsi mpaka za serikali.
Awali wakati akitoa shukrani zake aliwataka walimu wa shule zilizofanya vizuri kutojisahau kwa matokeo waliyoyapata badala yake waongeze bidii ili kufika mbali zaidi lakini pia alizitaka shule zilizofanya vibaya kuhakikisha zinafuta matokeo hayo katika mitihani ijayo na kwenda na kasi itakayowapelekea kwenda sambamba na juhudi za serikali za kukuza elimu nchini inayotambulika kama matokeo makubwa sasa.
Katika ghafla hiyo mkuu wa wilaya alikabidhi zawadi kwa shule zipatazo 13 zilizofanya vizuri na zile zilizofanya vibaya za msingi na sekondari ambapo kwa upand wa shule za msingi zilizofanya vizuri ni king david, rahaleo, na kambarage na zilizofanya vibaya ni LWELU, MITENGO, na likonde wakati za sekondari zilizofanya vizuri ni AQUINAS, MTWARA UFUNDI na SHANGANI na zilizofanya vibaya ni MANGAMBA huku shule zilizoboreka kitaaluma zikiwa mbili nazo ni shule ya sekondari CHUNO na shule ya sekondari ya NALIENDELE.

No comments:

Post a Comment