Madaktari na wauguzi mkoani Mtwara wametakiwa kutoa ushirikiano
na huduma bora kwa wagonjwa waliojiunga na mfuko wa hifadhi ya jamii wa (NSSF)
Mkoani Mtwara.
moja kati ya wagonjwa akiwa amelazwa katika Hospitali ya Ligula Mtwara |
Wito huo umetolewa na meneja wa mfuko wa huo mkoa wa
Mtwara Stanley Millanzi , wakati akizungumza na mwandishi wa habari wa kituo
hiki mapema leo ofisini kwake.
Millazi amesema kuwa kwa wananchama waliojiunga na mfuko
huo, wanaweza kupata huduma ya afya kwenye vituo vilivyo karibu na maeneo wanayoishi.Amezitaja sehemu zinazotoa huduma kwa wanachama hao kwa
Mkoa wa Mtwara, ambazo ni hospitali ya Rufaa ya Ligula pamoja na ndanda ndogo zote
katika Manispaa ya Mtwara ya Mikindani.
No comments:
Post a Comment