NA Shafii Mohamed ,Arusha
Timu ya soka ya AFC leo imetawazwa kuwa bingwa mpya michuani ya ligi ya taifa ngazi ya wilaya ya Arusha mjini kwa kujikusanyia jumla ya pointi10 katika hatua ya 6 bora ligi ambayo imeanza mnamo mwezi wa 7 kwa kushirikisha jumla ya timu 18 za jiji la Arusha.
michuano hiyo ambayo imefikia tamati leo kwa michezo mitatu ilio pigwa katika viwnja tofauti ,uwanja wa engutoto watoto wa mchezaji wa zamani rashid idd chama CIDT SC wametoka sare ya bila kufungana 0-0 dhidi ya SUYE SC hivyo kuifanya suye kushika nafasi ya pili kwa kujikusanyia pointi 7 katiaka round hii.
Katika uwanja wa shule ya sekondari ya ILBORU AFC wamepokea kipigo cha 1-0 kutoka kwa timu ya jeshi 977fc lakini kipigo hicho hakikuweza kuivua ubingwa AFC ambao tayali wamekwisha jihakikishia ubingwa huo kwa kushinda michezo mitatu na kutoa sare mchezo mmja na kufungwa mechi m0ja katika hatua ya 6 bora
Mchezo wa mwisho uliwakutanisha NYOTA SC almaarufu brazil wa Arusha kutoka maeneo ya daraja2 dhidi ya MALTI FLOWER FC katika awanja wa kukmbukumbu ya shekhe Amri Abeid na timu hizo kutoka sere ya kufungana 1-1 lakini sare hiyo ilikuwa balaa kwa timu zote mbili
Mbali na kuwa binngwa leo ikumbukwe AFC ilifanya vizuri sana katika hatua ya makundi kwa kumaliza ikiwa imejiksanyia pointi 16
Akizungumza na swacotz katibu wa chama cha mpira wilaya ya Arusha mjini Zakayo mjema amethibisha kuwa kwa matokeo hayo AFC pamoja n suye sc ndio timu ambazo zita wakirisha jiji la Arusha katika michuano ya ligi ya mkoa ambayo itaanza hivi karibuni
No comments:
Post a Comment