Wakimbizi kadhaa wanahofiwa kuwa wamekufa baada ya mashua yao kuzama karibu na kisiwa cha Sicily, katika bahari ya Mediterenia nchini Italia.
papa fransisco |
Watu 250 wanasemekana kuwa walikuwamo katika mashua hiyo iliyozama umbali wa maili 70, kutoka pwani ya kisiwa cha Italia cha Lampedusa. Shirika la Habari nchini Italia Ansa, limesema takribani miili 50 ikiwa ni pamoja na wanawake na karibu watoto 10, imeondolewa baharini.
Waziri Mkuu wa Italia Enrico Letta, amesema kiasi ya manusura 150 wameokolewa na meli nyingine ya Malta.
Wiki iliyopita wakimbizi zaidi ya mia tatu walikufa maji karibu na kisiwa hicho cha Lampedusa.Mashua hiyo iliyokuwa inawasafirisha wakimbizi mita tano ambao wengi wao ni kutoka Eritrea na Somalia ilizama baada ya kuwaka moto.
No comments:
Post a Comment