Umoja wa Mataifa umepanga kufanyika kikao chenye
shabaha ya kujadili maendeleo ya nchi za Kiafrika, huko Addis Ababa mji mkuu wa
nchi ya Ethiopia.
Kamati ya Uchumi wa Afrika katika Umoja wa Mataifa
imeeleza kuwa, kikao hicho kitaanza kufanyika Oktoba 31 mwaka huu.
Kamati hiyo ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia
uchumi wa Afrika imeeleza kuwa, kikao hicho kitaendelea hadi Novemba 5, na
kuzishirikisha Kamisheni ya Umoja wa Afrika na Benki ya Maendeleo ya Afrika.
Kamati ya Uchumi wa Afrika ya Umoja wa Mataifa
imeeleza kuwa, washiriki wa kikao hicho watafanya juhudi za kufikia kwenye
natija kuhusiana na mambo yanayopaswa kupewa kipaumbele ambayo yatakuwa chachu
ya maendeleo imara barani Afrika.
Kamati hiyo imeeleza kuwa, kikao hicho kitafanya
juhudi pia za kupata uungaji mkono na misaada ya nchi wafadhili zenye lengo la
kuboresha ustawi wa Afrika.
No comments:
Post a Comment