Uchaguzi wa Urais na Makamu wake katika chuo cha uandishi wa
habari Royal ulimalizika majira ya saa kumi n a moja jioni mara baada ya
shughuli ya kupigwa na kuhesabu kura iliyochukua takribani masaa matano ambapo
mwenyekiti wa tume ya uchaguzi chuoni hapo Bw:John Luhende alitangaza matokeo
ya uchaguzi huo na kuwataja washindi kama ifuatavyo
Jumla ya wapiga kura walioshiriki zoezi hilo walikuwa 215 na
katika matokeo hayo hakuna hata kura moja iliyoharibika hivyo basi matokeo
halisi kwa upande wa wagombea wa umakamu wa urais ni kwamba mgombea namba moja JUMA
MSIRI amepata kura 61 sawasawa na asilimia 28.3 na mgombea namba mbili DANIEL
KILEWO amepata kura 154 sawasawa na asilimia 71.6 ya kura zote hivyo mshindi ni
DANIEL KILEWO ndiye atakayekuwa makamu wa Rais wa Royal kwa mwaka 2013-2014
Kwa upande wa wagombea wa Urais mgombea namba moja SHANGWE
MZINGA amepata kura 101 sawasawa na asilimia 46.6 ya kura zote 215 zilizopigwa na mgombea namba mbili GEOFREY MTENZI amepata
kura 114 sawasawa nas asilimia 53.0 ya
kura zote zilizopigwa hivyo basi kwa matokeo hayo Bw: Geofrey Mtenzi
ametangazwa kuwa Rais wa Royal mwaka 2013-2014.
Washindi wanatarajiwa kuapishwa siku ya ijumaa ya tarehe
05/07/2013 huku mwenyekiti huyo akiwataka watu kuwa na hali ya utulivu na
kuyakubali matokeo hayo iwapo mtu hatoridhika atatkiwa kukata rufaa ya kupinga
matokeo ndani ya wiki mbili yaani siku kumi na nne toka kutangazwa kwa matokeo.
|
eneo la kutangazia matokeo likiwa limeandaliwa |
|
wanaroyal wakisubiri matokeo ya uchaguzi |
|
wajumbe wa tume ya uchaguzi wakitoka katika chumba cha kuhesabia kura tayari kwenda kutangaza matokeo |
|
masanduku yaliyohifadhiwa kura |
|
mwnyekiti wa tume katikati na katibu wake kushoto kulia ni mshauri wa tume |
|
wahesabuji kura wakisubiri kutangaza matokeo kushoto ni Rashidi Usi |
|
Mshauri wa tume akizungumza kitu na wanaroyal kabla ya kutangazwa kwa matokeo |
|
Mwanasheria wa tume ya uchaguzi akitoa shukrani |
|
mwenyekiti wa tume akitoa matokeo |
|
mshindi wa nafasi ya umakamu wa urais Daniel Kilewo |
|
mshindi wa nafasi ya urais akielekea kupongezwa |
|
Geofrey Mtenz Rais mpya Royal |
|
washindi wakipongezana |
PICHA ZA MATUKIO YA HARUSI YA KELVINI NA JAVINATA ILIYOFANYIKA JUMAMOSI YA TAREHE 30/06/2013 KATAKA UKUMBI WA STANLION GARDEN MIKOCHENI
|
JAVINATA NA MUMEWE KELVIN WAKINYWESHANA SHAMPEIGN |
No comments:
Post a Comment