Mama wa Kasarani ajiteketeza na wanawe juu ya mapenzi...
KESI YA LADY JAYDEE YAPIGWA KALENDA
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kinondoni, leo imeiaharisha kesi inayomkabili
msanii wa kizazi kipya nchini, Judith Wambura 'Lady Jaydee' a.k.a
Annaconda dhidi ya uongozi wa Clouds Media Group hadi Agosti 2, mwaka
huu.Kesi hiyo ya madai iliyopo mbele ya Hakimu Athumani
Nyamlani, leo ililetwa kwa ajili ya kusikilizwa lakini ilishindikana
kutokana na wakili anayemtetea, Jaydee kutotokea mahakamani hapo na
kumtuma mwakilishi wake.Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa wakili
huyo wa Jaydee, amekwenda katika Mahakama Kuu kuhudhuria kesi nyingine
na hivyo kushindwa kufika mahakamani hapo kuendelea na kesi hiyo na
hivyo kuahirishwa hadi Agosti 2, mwaka...
KANISA KATOLIKI PAROKIA YA URU LAKUMBWA NA MAMBO YA KISHIRIKINA ( UCHAWI )
HOFU kubwa imetawala Kanisa Katoliki Parokia ya Uru iliyopo Wilaya ya
Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro, kutokana na matukio kadhaa
yanayoendelea kutokea katika kanisa hilo huku baadhi ya watu
wakiyahusisha na imani za kishirikina.
Katekista wa parokia hiyo,
Lucian Tesha, aliwaambia waamini waliokusanyika katika ibada ya misa ya
kwanza kanisani hapo juzi Jumapili kuwa usalama katika kanisa hilo upo
shakani na kuwataka kuwa macho.
Hali hiyo inatokana na kile alichodai kuwa kuna mtu mmoja (mwanaume)
kwamba amekuwa akionekana eneo la kanisa akiweka vitu mbalimbali ambavyo
havina nia njema na kanisa hilo la Moyo Mtakatifu...
CHADEMA HAINA UBAVU WA KUMKATAA TENDWA
OFISI ya Msajili wa Vyama vya Siasa, imesema Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (Chadema) hakina ubavu wa kumkataa au kutomtambua John Tendwa
kuwa ndiye msajili wa vyama vya siasa nchini.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Naibu Msajili wa Vyama vya Siasai,
Rajab Baraka alipozungumza na MTANZANIA kuhusu kauli iliyotolewa na
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa aliyedai chama hicho
hakimtambui John Tendwa kuwa ndiye msajili wa vyama vya siasa.Katika
madai yake Dk. Slaa alidai Tendwa anakipendelea CCM katika kutoa haki
ya demokrasia na hatendi haki kama mlezi wa vyama vyote vya siasa
nchini.Dk. Slaa alisema hayo wiki iliyopita alipokuwa...
No comments:
Post a Comment