Rais Jakaya Kikwete amefanya
mazungumzo kwa njia ya simu na Rais wa Sudan, Omar Bashir, kuhusu kuuawa
na kujeruhiwa kwa askari wa Tanzania, walioko katika ulinzi wa
kimataifa wa amani katika jimbo la Darfur.
Taarifa ya
Ikulu iliyotumwa kwa vyombo vya habari jana, imeeleza kuwa katika
mazungumzo hayo, Rais Kikwete alimtaka Rais Bashir kuchukua hatua za
haraka kuwasaka na kuwakamata waliohusika na kitendo hicho kiovu, na
kuwafikisha mbele ya sheria haraka iwezekanavyo.
Rais Bashir
amekubaliana na Rais Kikwete na kumuahidi kuwasaka hadi kuwakamata wale
wote waliohusika na kuwachukulia hatua za kisheria.
Alimueleza Rais
Kikwete...
MZEE MANDELA ASHEREHEKEA MIAKA 95 LEO HUKU AKIWA MAHUTUTI HOSPITALINI
Afrika Kusini leo wanasherehekea
miaka 95 ya kuzaliwa kwa Mzee Nelson Mandela huku rais huyo wa zamani
bado yuko mahututi hospitalini.
Ilikuwa
ikitabiriwa kwamba shujaa huyo wa vita dhidi ya ubaguzi wa rangi kwamba
angeruhusiwa kwenda kusherehekea siku yake ya kuzaliwa lakini bado yuko
hospitali kutokana na kurejea maambukizi kwenye mapafu.
Kituo cha
Kumbukumbu ya Nelson Mandela na makundi mengine yamewataka watu
kujitolea kwa dakika 67 kwa kazi za hisani kukumbukia miaka 67 ambayo
Mandela aliitumikia jamii yake.
Umoja wa Mataifa pia umetambua
mapambano ya Mandela dhidi ya ubaguzi wa rangi na kusema siku yake ya
kuzaliwa ni fursa...
No comments:
Post a Comment