KOCHA wa wageni wa Ligi,Timu ya Stand United Emmanuel Masawe
amesema atatumia michezo minane ya Kirafiki kukitambua kikosi hicho kabla ya
kuanza Ligi kuu Tanzania Bara mwaka huu.
Stand United,Polisi Morogoro na Ndanda Fc zimepanda ligi Kuu Tanzania
Bara Msimu huu, zikichukua nafasi ya Rhino Rangers,JKT Oljoro na Ashanti
United.
Kocha huyo alisema ,kuwa atatumia mechi nane ilikutoa tathmini ya
kikosi chake ambacho anaamini kitaleta upinzani zaidi ya Mbeya City mwaka jana.
Alisema Kikosi hicho kitajipima na timu za kanada ya ziwa dhidi
ya Toto Africa ya
mwanza na Geita Veterani Fc,kabla ya kuja Mkoani Morogoro kucheza na Mtibwa
Sugar na Polisi Morogoro kama watahitaji kupijipima nao nguvu.
Pia ,alisema watacheza na JKT Ruvu,Ndanda Fc na timu mmoja jiji
Dar es Salaam na watahitimisha na Azam Fc kwenye Uwanja Kambarage mjini
Shinyanga.
Alitaja pia idadi ya mechi watakazozicheza kuwa ni michezo nane ya kirafiki kabla ya kuanza ligi
kuu msimu huu,na watacheza na Geita Veterani,Toto Africa,Mtibwa Sugar,Polisi
Moro,JKT Ruvu,kama Ndanda Fc watahitaji kucheza na wao watacheza nao,pamoja na
Azam fc

No comments:
Post a Comment