EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Thursday, January 16, 2014

KOMBE LA DUNIA-BRAZIL 2014: ENGLAND KUJIPIMA NA ‘WALATINO!’




BRAZIL_2014_LOGO
































ENGLAND, ambayo iko Kundi D la Fainali za Kombe la Dunia pamoja na Italy, Uruguay na Costa Rica, imeandaa Mechi 3 za Kirafiki kabla yaENGLAND_IN_WEMBLEYFainali hizo dhidi ya Timu toka Marekani ya Kusini na ya Kati ili kujizoeza kwa mapambano yao na Uruguay na Costa Rica.
FA, Chama cha Soka England, kimetangaza kuwa England itacheza na Peru Uwanjani Wembley Jijini London hapo Mei 30 na kisha Kikosi chao kitasafiri kwenda Miami, Florida kitakapopiga Kambi ya mwisho kabla kwenda Brazil ili kujizoeza na Hali ya Hewa ya Joto.
Huko Miami, England itacheza na Ecuador hapo Juni 4 na kufuatia Mechi na Honduras Juni 7 zote zikichezwa Sunlife Stadium.
Akiongelea Mechi hizo, Kocha wa England, Roy Hodgson, amesema: “Nimefurahi kwa kupata Mechi hizi na maandalizi yetu kuelekea Fainali za Kombe la Dunia kwa ujumla. Niliwaambia wazi FA nataka Timu kutoka Marekani ya Kusini na ya Kati na wamefanikiwa kutuletea!”


KOMBE LA DUNIA-BRAZIL 2014
England=Kundi D:
RATIBA:
-Juni 14: v Italy
-Juni 19: v Uruguay
-Juni 24: v Costa Rica

Hodgson anatarajiwa kuteua Kikosi cha awali cha Kombe la Dunia chenye Wachezaji 30 karibu na Mei 13 na kisha England itapiga Kambi huko Portugal kwenye Wiki ambayo itapakana na Fainali ya FA CUP Uwanjani Wembley na Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI itakayochezwa Lisbon, Portugal hapo Mei 24.
Baada kucheza na Peru hapo Mei 30 Uwanjani Wembley, Kikosi cha England kitapunguzwa hadi Wachezaji 23 ambayo ndio idadi inayoruhusiwa kwa Fainali za Kombe la Dunia.
Baada Mechi zake huko Miami, England itasafiri kwenda Rio De Janeiro, Brazil ambako ndiko itakaa kabla kusafiri kwenda Mji wa Manaus Siku 2 kabla kuivaa Italy Mjini humo hapo Juni 14 katika Mechi yao ya Kwanza ya Kundi D.

No comments:

Post a Comment