Dodoma.
Kutokana na hali hiyo waziri huyo alionekana kama
anawasilisha bajeti ya wizara yake mbele ya viti vitupu vilivyopo katika
ukumbi huo. Wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano ni 355,
wakiwemo mawaziri na naibu mawaziri 55.
Vikao vya Bunge la Bajeti vinavyoendelea mjini
hapa huanza saa tatu asubuhi hadi saa saba mchana na kuendelea tena
kuanzia saa 11 jioni hadi saa mbili usiku. Kombani aliwasilisha bajeti
hiyo saa 10 jioni ambapo mpaka anamaliza kuisoma saa 11 jioni, idadi ya
wabunge waliokuwepo katika ukumbi huo ilifikia 87, huku wakiongezeka
mawaziri sita tu na kufanya idadi yao kufikia 11.
Mpaka inafika saa 10:15 jioni idadi ya wabunge
iliongezeka na kufikia 24 wakiwemo mawaziri hao, dakika 20 baadaye idadi
yao iliongezeka tena na kufikia wabunge 38.
Licha ya uchache wao baadhi yao walikuwa hawatulii
eneo moja, kwani walikuwa wakihama hama huku wakionekana kujadiliana
jambo na wenzao.
Mpaka Kombani anamaliza kuwasilisha bajeti yake,
saa 11:05 idadi ya wabunge waliokuwa katika ukumbi huo ilifikia 87,
wakiwamo mawaziri hao.
Pamoja na uchache huo bajeti ya wizara hiyo
ilipitishwa juzi hiyo hiyo licha ya mbunge wa Mbozi Magharibi (Chadema),
David Silinde kumtaka Spika wa Bunge, Anne Makinda kuzingatia akidi ya
wabunge kwa madai kuwa ni ndogo kupitisha bajeti hiyo.
Hata hivyo, Spika Makinda alisema akidi hiyo siyo
tatizo na kusisitiza kuwa huwa inazingatiwa zaidi wakati wa kupitisha
bajeti kuu kwa maelezo kuwa kila mjumbe huitwa kwa jina lake katika
upitishwaji huo.
Akitoa ufafanuzi kuhusu utoro wa wabunge Katibu wa
Bunge, Dk. Thomas Kashilillah alisema kuwa akidi ya wabunge huzingatiwa
zaidi kama kutakuwa na kikao cha kutoa uamuzi.
“Kama kuna kikao cha kutoa uamuzi ni lazima tuangalie akidi lakini kama ni vikao vya kawaida hukuna tatizo lolote” alisema.SOURCE>>>>MWANANCHI
No comments:
Post a Comment