NA
MWANDISHI WETU
KAMPUNI ya Bia ya Serengeti (SBL) inatarajia wiki hii kupata
mshindi wake wa kwanza wa safari ya Brazil katika droo yake ya nne ya Winda
safari ya Brazil na Serengeti.
Hadi sasa washindi mbalimbali wamejishindia zawadi ikiwemo ving’amuzi, ipad, bia za bure, na
fedha taslimu.
Mshindi huyo wa safari ya Brazil atalipiwa gharama zote ambapo
atatembelea vivutio mbalimbali nchini humo.
Meneja wa Bia ya Serengeti Rodney Rugambo alisema juzi jijini
Dar es Salaam kuwa mpaka sasa washindi watano wamejishindia simu aina ya
Samsung Galaxy Tab na wengine 18 wameshinda
ving’amuzi kupitia promosheni hiyo.
ving’amuzi kupitia promosheni hiyo.
“Tunapenda kuwaambia wateja wetu kuwa wiki hii kutakuwa na
droo kubwa yakupata mshindi wa kwanza wa safari ya Brazili ambaye atalipiwa
gharama zote na Kampuni ya Bia ya Serengeti.
“Zawadi hii kubwa ni kwa ajili ya wateja wetu na cha kufanya ili
kushinda zawadi na safari hiyo ni kufungua bia yako ya Serengeti kokote nchini
na kufuatilia maelezo ya promosheni na unaweza kuwa mshindi wetu wa wiki
inayokuja,” alisema.
Mmoja wa washindi wa simu ya Samsung Tab, Vedastus Kalinga
kutoka Mbeya, aliishukuru SBL na kusema amefarijika kupata zawadi hiyo itakayomsaidia
kufanya vitu vyake kwa urahisi zaidi katika ulimwengu huu wa dijitali licha ya
kuwa ndoto yake ni kupata safari ya kwenda Brazil.
No comments:
Post a Comment