EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Thursday, March 6, 2014

BONDIA MWAKASANGA 'SHOKA' AJIANDAA NA PAMBANO LA UZITO WA JUU

 
NA msham ngojwika ...dAR ES SALAAM
 BONDIA Bernard Mwakasanga 'Shoka ya Bucha ' ameingia kambini kwa ajili ya kujiandaa na mpambano lisilokuwa la ubingwa uzito wa juu dhidi ya Iddi Kipandu utakaofanyika wa March 23 mwaka huu kwenye Ukumbi wa Friends Corner Manzese, Dar es salaam.
Mpambano huo ambao unasubiliwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa masumbwi, homa yake imezidi kupamba moto baada ya kila mmoja kumtambia mwenzake kuwa atammaliza raundi za awali.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana Mwakasanga alisema Bonge ni kama nyama ya bucha hivyo ajiandae kumuondoa kwenye raundi ya kwanwa ya mpambano huo.
Mratibu wa mpambano huo Waziri Rosta alisem kuwa mpambano huo utakuwa na mapambano mengine kadhaa ya utangulizi ambapo bondia Fadhili Mjia 'Stoper' ataonyeshana ubabe na Juma Selemani huku Twalibu Mchanjo akikutana na Mohamed Babeshi.
Wengine ni Hassani Mandula akipambana na Ally Bugingo mpambano mwingine utawakutanisha Amani Bariki na Selemani Motto, Halidi Manjee akioneshana umwamba na Shabani Mtengela huku Mustafa Dotto akizichapa na Ismail Ndende na Salimu Chagogo atapigana na Salumu Kombe.

Rosta alisema kuwa ulinzi na usalama utakuwa wa kutosha katika mpambano huo ili kuwapa fursa majaji kutoa maamuzi ya haki na usawa.

No comments:

Post a Comment