MUIMBAJI mahiri wa muziki wa dansi
Nchini Muumini Mwinjuma ‘Kocha wa Dunia’ amejipanga kuwafunika nguli wenzake
Ally Choki na Ramadhani Masanja ‘Banza stone’ katika uzinduzi wa albamu ya
Mtenda akitendewa ya bendi ya Extra bongo utakaofanyika Februari 22 katika
ukumbi wa Dar live, Mbagala.
mwinjuma muumin
Uzinduzi huo unaenda sambamba na
albamu ya Mkurugenzi wa bendi hiyo Ally Choki iliyo katika mtindo wa Rhumba
akiwa amewashirikisha wanamuziki mbalimbali nchini wa dansi, Bongo fleva, Hip
hop na Taarabu.
Akizungumza na DIMBA jana, Muumini
alisema anawaonea huruma sana wanamuziki hao kwani ni lazima atawafunika katika
uzinduzi huo na watajuta kumualika.
mwinjuma ndani ya kazi
“Nimealikwa kusindikiza tu lakini
watajutia uamuzi wao huo kwani ni lazima ni wafunike nadhani wote wananijua
uwezo wangu na huwa sifanyi makosa katika shoo kama hizi hivyo wajiandae kuwa
nyuma yangu,” alisema.
banza stone atakinukisha dar live
banza na Alliy Choki wote watakinukisha Dar live
Aliongeza kuwa baada ya kufanya
makubwa katika uzinduzi huo ndipo ataelekeza nguvu katika kutangaza wanamuziki
wake wapya atakaokuwa nao katika bendi
yake huko itakayokuwa na maskani yake mjini Kahama.




No comments:
Post a Comment