huku ndiko iliko azam fc
Katibu Wa Azam FC, Nassor Idrisa ‘Father’ Ameiambia Swacotz Mchana Jana
Kutoka Beira Kwamba Timu Imefikia Katika Hoteli Ya Rainbow Na Mechi Itachezwa Jumapili
Saa 8:00 Mchana Kwa Saa Za Msumbiji Na Saa 10:00 Jioni Kwa Saa Za Afrika
Mashariki.
Father Amesema Mchezo Huo Utaonyeshwa Moja Kwa Moja Na Televisheni Ya Azam TV.
“Lakini Mvua Kubwa Inanyesha Huku, Inanyesha Kutwa Nzima, Ila Maandalizi Ni
Mazuri Na Tumekuja Na Viatu Vya Kuchezea Kwenye Mvua, Hivyo Tupo
Kamili,”Alisema Father.
Azam FC Iliyoanza Kwa Ushindi Mwembamba Wa 1-0 Jumapili Uwanja Wa Azam Complex
Jumapili, Iliondoka Jana Asubuhi Dar Es Salaam Kwa Ndege Ya Fast Jet Hadi Johannesburg,
Afrika Kusini Ambako Waliunganisha Ndege Ya Shirika La Msumbiji Kwenda Beira.

Azam Imeondoka Na Wachezaji 21 Ambao Ni Makipa; Mwadini Ali, Aishi Manula Na Jackson
Wandwi, Mabeki Luckson Kakolaki, Erasto Nyoni, Malika Ndeule, Aggrey Morris, Said
Mourad, David Mwantika, Viungo Ibrahim Mwaipopo, Kipre Balou, Jabir Aziz, Salum
Abubakar, Himid Mao, Khamis Mcha Na Washambuliaji John Bocco, Kipre Tchetche, Brian
Umony, Seif Abdallah, Gaudence Mwaikimba Na Ismael Kone.
No comments:
Post a Comment